KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, June 28, 2012

Pre-season :Manchester United vs Barcelona nchini Sweden.

Sir Alex Furguson akiwa na mtendaji mkuu wa United David Gill

Manchester United imetangaza kutaka kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Barcelona mchezo wa maandalizi ya kuanza msimu mpya wa ligi “pre-season” mjini Gothenburg chini Sweden.
Mchezo huu umepangwa kufanyika jumatano August 8 uwanja wa Ullevi ambao ulitumika katika mchezo wa fainali ya UEFA 2004.
Mtendaji mkuu wa United David Gill amekaririwa kupitia mtandao wa klabu hiyo akisema
"mchezo baina ya Manchester United dhidi ya Barcelona ni mchezo mkubwa katika soka duniani hivyo tunajisikia faraja kufanya kazi na GotEvent kufanikisha mchezo huu katika mji mzuri kama Gothenburg.
"tuna mashabiki wetu wengi katika ukanda wa nchi za  Scandinavia na ni mchezo ambao utakuwa katika sehemu ya kujiandaa kwa msimu mpya."
Mara ya mwisho kwa timu hizo kukutana ilikuwa July 30 2011 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika FedEx field jijini Washington nchini Marekani na United ikashinda kwa mabao 2-1 mabao yakifungwa na Michael Owen.

No comments:

Post a Comment