Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) limemtambulisha rasmi leo mbele ya waandishi wa habari kocha mpya
wa timu za Taifa za vijana, Jakob Michelsen kutoka Denmark ambaye amechukua
nafasi ya Kim Poulsen ambaye hivi sasa anainoa Taifa Stars.
Michelsen ambaye amepewa
mkataba wa mwaka mmoja alitambulishwa na Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah na
kusema falsafa yake ni kama ile ya Poulsen ya kumiliki mpira na kushambulia muda
wote wa mchezo.
Kabla ya kuja Tanzania,
Michelsen alikuwa kocha wa timu ya daraja la kwanza ya Hobro IK ya Denmark. Ana
leseni A ya ukocha kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA), leseni ya
ukocha wa vijana kutoka Chama cha Mpira wa Miguu cha Denmark (DBU).
Moja ya mafanikio yake ni
kuipa ubingwa wa Denmark, timu ya Skovbakken kwenye ligi ya timu zenye umri
chini ya miaka 18. Ubingwa huo aliupata msimu wa 2005/2006
No comments:
Post a Comment