KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, December 5, 2013

Carlo Ancelotti anasema 'Xabi Alonzo ndiye atakayenipa sikukuu ya Christmas'

Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti ana matumaini kuwa Xabi Alonzo atampa kipindi kizuri cha sikukuu ya Christmas kwa kusajili mkataba mpya.

Kiungo huyo mchezeshaji kwasasa mkataba wake unaelekea kumalizika baada ya msimu lakini Ancelotti amesisitiza kuwa Alonso anasalia kuwa mchezaji muhimu ndani ya Madrid na ana matumaini kuwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 atasaini mkataba wa kuendelea kusalia hapo kabla ya mwaka kumalizika.

"Ningependa Xabi Alonso asaini mkataba mpya ili niwe na furaha wakati wa sikukuu".

"Ni kiungo muhimu kwa Madrid. Ana uzoefu na ubora na ni muhimu ndani ya timu.

"Xabi Alonso ananikumbusha kiasi mimi mwenye ingawa anapiga pasi nzuri na ni fundi wa mbinu."

Ancelotti pia akaendelea mbele zaidi kwa kuweka wazi kuwa Cristiano Ronaldo atasalia kuwa chagua lake la kwanza kwa kupiga mipira iliyokufa licha ya kwamba Gareth Bale alipiga mpira mzuri katika mchezo dhidi ya Galatasaray.

"Cristiano remains the first choice. Bale also agrees that Ronaldo is our best bet for free kicks from close range."

Madrid inajiwinda na mchezo wa Jumamosi wa Copa del Rey dhidi ya Olimpic de Xativa.

No comments:

Post a Comment