KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, December 6, 2013

Nelson Rolihlahla Mandela: was the heavyweight boxer



Nelson Mandela alianza kujihusisha na mchezo wa ndondi mwaka 1936 katika Chuo Kikuu cha Fort Hare. Wakati huo akiwa ni kijana kutoka katika kabila la  Xhosa.

 Alijiunga na taasisi ya wasomi weusi huko Alice , Eastern Cape kwa ajili ya kusomea shahada ya Sanaa , na kujifunza  Kiingereza , utu, siasa, mambo ya utawala na sheria za kidachi na Kirumi. Ingawa alizungukwa na wanaharakati na marafiki wengi wanaohusika na ANC, Mandela alijiweka mbali nao akiendelea kutunga kutunga itikadi yake mwenyewe.

 Shughuli zake kubwa zilikuwa ni mambo ya imani yake ya Kikristo na kusoma zaidi Biblia na kujifunza mchezo wa ngumi yaani ndondi .
Nelson Mandela akiwa kama mwanamasumbwi alianza kuwa ulingoni kabla ya kuanza harakati za kupigana na siasa haramu za ubaguzi wa rangi.
Kama mwanamichezo mara zote alitumia muda wake katika mazoezi kwa kunyanyua vitu vizito na kukimbia umbali mrefu kwa ajili ya kupunguza uzito na pia akishiriki katika michezo ya mipira ya ndani.
Alipoanza kukomaa zaidi kiumri, Mandela alielekea Johannesburg kusomea masomo ya sheria katika chuo cha Whitwatersrand mwaka 1943, na alikuwa ni mwanafunzi pekee mwenye asili ya kiafrika na hapo ndipo alipoaanza kuumizwa na ubaguzi kwani kilikuwa ni kipindi ambacho ubaguzi wa rangi ulikuwa kwa kiwango cha juu na kulikuwepo na mvutano mkubwa juu ya ubaguzi wa rangi.

Nelson Mandela akiwa chuoni hapo alishindwa kutumia kituo cha mazoezi cha chuo hicho na ndipo alipolazimika kusafiri kutafuta kituo mbadala cha kufanyia mazoezi yake ya ngumi  ambapo alijiunga katika kituo kimoja cha kijamii yaani
Community Centre) katika kitongoji kikubwa cha jiji la  Johannesburg  Soweto YMCA.

Ndani ya kituo hicho ambacho baadaye kilikuwa maarufu sana ambapo hasa baadaye wasanii wakubwa na wanaharakati walikuwa wakikitumia kufanya burudani zao wasanii kama Miriam Makeba na Brenda Fassie.

 Kituo hicho mara kwa mara kilitumika kama sehemu ya kuchonga mizinga ya kupambana na ubaguzi wa rangi kwa kuwakutanisha wanaharakati.

Lakini kwa Mandela, kucheza ngumi haikuwa na maana sana kwake alitumia mchezo huo kama njia ya kuondokana na hila za kibaguzi na kuleta ukombozi wa kisiasa ambapo baadaye aliandika autobiography 'Safari ndefu kuelekea ukombozi ambapo ndani yake alielezea kwa jinsi gani alivyokuwa hafurahii unyanyasaji kama ilivyo kwenye mchezo wa ndondi ambao sayansi yake ianavyoeleza.

 Alieleza jinsi sayansi ya ndondi ilivyo ya ajabu ambapo mtu alikuwa akitumia mwili wake kujilinda na wakati huohuo anashambulia na kurudi nyuma.

Nelson Mandela, boxer: fought in the ring before he fought apartheid
Ndani ya kipindi hicho cha ubaguzi wa kiwango cha juu Mandela alishangazwa na jinsi ambavyo ubaguzi ulivyokuwa kama taasisi na ndipo Mandela alipoanza taratibu kuwa mwanasiasa
Nelson Mandela, boxer: fought in the ring before he fought apartheid 
Kituo hicho baadaye kiligeuka kuwa kitovu cha wanaharakati wa upinzani wa ubaguzi wa rangi ambacho wasanii kama Miriam Makeba na marehemu Brenda Fassie walikuwa wakifanya maonyesho yao hapo. Lakini kwa Mandela, mchezo wa ngumi haukuwa ni kupigana lakini ilikuwa ni aina ya uundwaji wa maandalizi ya kujiondoa na hila za kibaguzi. Baadaye alindika autobiography ‘The Long Walk to Freedaom’, akiandika zaidi kuwa sikufurahia mapambano ya ngumki kwa kiwango kikubwa kama ilivyo sayansi yake.  Nilikuwa nina kiu ya kujua vipi mtu anatumia mwili wa mwenzake kujilinda, vipi mtu anatumia mkakati wake kushambulia na kurudia tena kutenda hilo.

‘Boxing is egalitarian.  In the ring, rank, age, colour, and wealth are irrelevant . . . I never did any real fighting after I entered politics.  My main interest was in training; I found the rigorous exercise to be an excellent outlet for tension and stress.  After a strenuous workout, I felt both mentally and physically lighter.  It was a way of losing myself in something that was not the struggle.  After an evening’s workout I would wake up the next morning feeling strong and refreshed, ready to take up the fight again.’
Nelson Mandela, boxer: fought in the ring before he fought apartheid 
Kuna moja ya picha maarufu ambayo mara ngingi imekuwa ikitumika kumuelezea Mandela kama mwanamichezo hususani ngumi alikuwa akifanya 'sparring' na nyota wa ngumi za kulipwa Jerry Moloi na hiyo ilikuwa ni mwaka 1953, huko Soweto.

Ilikuwa ni mwaka huo huo Mandela alifungua kituo cha sheria akiwa pamoja na Oliver Tambo, ambacho kilikuwa kituo pekee cha kisheria cha waafrika nchini humo.

Mwaka uliofuata Mandela aliaanza kutumikia mwaka wake wa kwanza jela katika hukumu ya kwenda jela miaka mitano kutoka na kuhamasisha wafanyakazi wa kiafrika kugoma na kuondoka nchini humo bila ruhusa .

Miaka miwili baadaye alishitakiwa kwa makosa ya njama za kutaka kuipindua serikali ya kibaguzi na makosa mengine manne ya hujuma na uhaini. Baada ya miezi minane alikutwa na hatia na ndipo alipowekwa ndani kwa miaka 25

Katika kesi yake Mandela alitamka maneno ambayo sasa yamekuwa yakitumika kama kipande maarufu cha hotuba zake

"Mimi nimekuwa nikichochea wazo la kidemokrasia ndani ya jamii ambapo ndani yake watu wataishi kwa pamoja na amani na kupata fursa sawa. Ni wazo bora ambalo natumaini kuishi hivyo na kwa mafanikio. Lakini kama hitajio la wazo langu ni hilo basi mimi niko tayari kufa. "

Nelson Mandela, boxer: fought in the ring before he fought apartheid 
Baada ya mandela kuachiwa huru na kuchaguliwa kuwa Rais wa kwanza wa Afrika kusini alitumia nguvu ya michezo kuunganisha watu wake waliokuwa katika hali ya mgawanyiko wa kibaguzi.

Mwaka 1995 nchini Afrika kusini kulifanyika fainali za kombe la dunia za mchezo wa Rugby ambapo nchi ilikuwa tofauti sana haijaunganishwa vizuri kutokana na kubaguana Mandela alitumia rugby kuunganisha wananchi wa kabila la Afrikana na wazalendo na kuanza safari ndefu ya kujenga upya taifa hilo

Kilikuwa ni kipindi cha mafaniko makubwa sana katika historia ya michezo ndani ya nchi hiyo ambapo mwandishi maarufu John Carlin maneno yafuatayo

 ‘Playing the Enemy: Nelson Mandela and the Game That Made a Nation’. 
YMCA cha Soweto bado kinaendelea na shughuli zake mpaka sasa na hakijabadilishwa tangu wakati huo Mandela akitumia kufanya mazoeizi yake ya ngumi.

 Madiba amekuwa kivutio kwa vijana wengi wa Afrika kusini kutaka kuvaa gloves na katika kituo cha mazoezi cha DO, bado wanatumia vyuma na vifaa vingine vizito ambavyo Mandela alitumia kubeba.

No comments:

Post a Comment