KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 27, 2012

AZAM YAPONGEZWA NA CECAFA KUTINGA FAINALI YA CECAFA.

Kikosi kamili cha timu ya Azam katika picha ya pamoja

Baraza la vyama vya soka Afrika mashariki na kati CECAFA limeipongeza klabu ya Azam kwa kufanikiwa kushiriki kwa mara ya kwanza na hatimaye kutinga fainali ya michuano ya vilabu bingwa inayoendelea hivi sasa jijini  Dar es Salaam kwa mara ya kwanza katika historia ya michuano hiyo.
Kauli hiyo ya pongezi imetolewa na katibu mkuu wa baraza hilo Nikolaus Musonye hii leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za shirikisho la soka hapa nchini TFF.
Pamoja na pongezi hizo kwa Azam CECAFA pia imesema timu zote zilizofika fainali zimefika hapo kihalali na kwamba hakuna timu iliyobebwa na kwamba kila timu Yanga ambao ndio mabingwa watetezi na Azam zote zimefika hapo kwa uwezo wao.
Azam na Yanga kesho zitakuwa zikiingia katika mchezo wa fainali ambao utaanza kupigwa saa kumi kamili jioni huku mchezo wa kusaka mshindi wa tatu ukipangwa kuanza saa saba kamili mchana.
CECAFA imesema viingilio vya mchezo wa kesho vitabaki kama ilivyokuwa katika michezo ya nusu fainali yaani  sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
CECAFA pia imetoa pongezi kwa serikali kwa kuwapa huduma zote zinazostahili za uwanja lakini pia pongezi nyingine zikienda kwa mashabiki ambao wameendelea kushangilia timu za kwa ustaarabu na nidhamu kubwa.

No comments:

Post a Comment