KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, July 14, 2012

DROGBA KAMA MFALME HUKO CHINA



Mashabaka wa kandanda nchini China wamkaribisha  Didier Drogba Shanghai
Nyota wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba amewasili nchini China na akipokewa kwa furaha na mashabiki wa kandanda nchini humo kwa ajili ya kuingia mkataba na klabu ya Shanghai Shenhua.
Mashabiki mamia kwa maelfu wa timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya soka wa klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya China wamempokea mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 34 kwenurv uwanja wa ndege wa Shanghai Pudong airport.
Drogba imeripotiwa kuwa atakuwa akipokea mshahara wa dolari za kimarekani $300,000 (£193,000) kwa wiki na kumfanya kuwa ni mmoja wa wachezaji soka wanaolipwa pesa nyingi duniani.
Drogba ni miongoni mwa wachezaji wengi wa kigeni ambao wameelekea nchini China.
Anajiunga na Nicolas Anelka katika klabu ya Shanghai Shenhua.

Baada ya kuwasili akiongea  Drogba amesisitiza kuwa hakwenda huko kwa ajili ya pesa.
Amesema
"ingekuwa rahisi kwake kuendelea kusalia ulaya , lakini nimechagua China. Pesa si kitu muhimu sana nipo hapa kwa ajili ya kusambaza uzoefu wangu."
Mamia ya mashabiki wamempokea Drogba katika uwanja wa ndege wa Shanghai wa Pudong hii leo.

No comments:

Post a Comment