KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 3, 2012

Maradona : Hakuna wa kuifunga Spanish machine

Diego Maradona

Mwasisi wa soka la Argentina Diego Maradona anaamini na kupigilia msumari kuwa timu ya taifa ya Hispania ya sasa haifungiki na ni timu kihistoria.
Maneno yake yanakuja baada ya kisago cha haja kwa timu ya taifa ya Italia cha mabao 4-0 chini ya Vicente del Bosque katika mchezo wa fainali ya mataifa ya Ulaya 2012.
Huo ulikuwa ni ushindi ambao ulitengeneza rekodi kwa Hispania kushinda mataji matatu makubwa duniani mfulilizo ikiwa ni mara ya kwanza kutokea duniani timu ya taifa kupata mafanikio makubwa kiasi hicho.
Maradona ambaye kwasasa ni meneja wa klabu ya Al Wasl ya Dubai anaamini La Roja ilistahili ubingwa huo kufuatia kutawala michezo karibu yote iliyocheza katika fainaali za majira haya ya kiangazi katika miji ya Poland na Ukraine.
Katika ukurasa wake katika gazeti la ‘Times of India’ Maradona ameandika
“[Spain] imedhihirisha wazi kuwa si tu timu bora ya taifa duniani lakini pia ni bora katika kucheza soka dunaini.
“hakuna wakuifunga ‘Spanish machine’. Cristiano Ronaldo alijaribu akiwa na Ureno lakini Hispania ilimdhibiti.
“[Andrea] Pirlo alijaribu na Hispania ilimdhibiti kwa kutumia wachezaji wanne waliomzunguka”

No comments:

Post a Comment