KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 22, 2012

Ramsey anamatumaini Van Persie atasalia Arsenal


Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey bado ana matumaini kwamba nahodha wake  Robin van Persie ataendelea kuwepo Emirates Stadium baada ya msimu wa uhamisho kumalizika.
Kumekuwepo na fununu juu ya hatma ya mduchi huyo  tangu alipotangaza kuwa hana mpango wa kujisajili tena na washika mitutu hao huku akikosoa sera za usajili za klabu hiyo na mwelekeo wa klabu hiyo.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28 aliifungia Arsenal jumla ya magoli 30 msimu uliopita na kuipa nafasi kikosi cha meneja Arsene Wenger kushika nafasi ya tatu katika ligi kuu ya nchini Uingereza.
Kiungo Ramsey ambaye kwasasa anajiwinda na Olympics akiwa katika kikosi cha Great Britain anafikiri kuwa itakuwa kupata mtu muafaka atakaye weza kufunga magoli hayo ya Van Persie endapo ataondoka.
Akoongea na Belfast Telegraph amenukuliwa akisema
"hatujui nini kinaendelea lakini tuna matuini kuwa atakuwepo Arsenal.
"alikuwa na msimu mzuri msimu uliopita na ni mchezaji mkubwa kwetu hivyo tuna matumaini atasalia."
Arsenal tayari imewasajili washambuliaji Lukas Podolski na Olivier Giroud pengine ni kutokana na kile kinachoonekana kutaka kuondoka kwa Van Persie.
Kuanza vibaya kwa msimu kwa klabu hiyo kunaonekana pengine kulisababishwa na Wenger kuacha kufanya usajili wakueleweka mapaka dakika ya mwisho wa uhamisho unamalizika.
Ramsey anaamini kuwa endapo biashara ingekwenda vizuri tangu mapema basi pengine wangeanza msimu vizuri kampeni yao nap engine kupunguza pengo kubwa la points 19 kati yao na wale waliokamata nafasi ya pili Manchester United.

No comments:

Post a Comment