KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, February 5, 2013

KIM POULSEN:'UMOJA NI NGUVU' AMALIZIA MAZOEZI UWANJA WA TAIFA KAMBA YA KUWAVAA CAMEROON KESHO.

Jumla ya wachezaji 20 wa timu ya taifa ya tanzani jioni ya leo wameshiriki mazoezi ya timu hiyo ukiacha cholo ambaye ni majeruhi .
Mazoezi hayo yalioanza saa 11:30 yamemalizika saa 12:00 jiioni ambapo wachezaji walikuwa wakifurahia mazopezi hayo huku wakionyesha ari kubwa ya kuinyoa Cameroon hapo kesho.
Akiongea mchana wa leo Poulsen amesema wachezaji wake wako tayari kwa mchezo huo ambapo amesema katika mchezo huo amewaagiza wachezaji kucheza kwa kasi, kujiamini na ikiwa ni pamoja na kutenganeza nafasi na hatimaye kufunga magoli.
Amesema licha ya kwamba Cameroon inawachezaji wenye uzoefu, nguvu na malengo bado Stars inanafasi ya kufanya vizuri endapo watacheza kwa nafasi , mchezo wa kasi, kutengeneza nafasi na hatimaye kufunga magoli.
Poulsena amesema amefurahia sana kupata mchezo huo ambao ameuita kuwa ni mchezo dhidi ya timu ngumu kama Cameroon baada ya jitihada za pamoja baina ya TFF na wadhamini wa Stars Kilimanjaro na angependa kupata michezo zaidi ya aina hiyo.
Kuhusu mchezo wa kesho amewataka wachezaji kucheza kwa kujiamini na kuonyesha uwezo wao wote. Anaamini katika njia ambayo anapita katika kuelekea kutafuta mwelekeo mzuri wa mafanikio ya timu na anaamini kwa kushirikiana kwa pamoja mafanikio yako karibu kama mwenyewe anavyopenda kuitumia kauli mbiu ya ‘Umoja ni nguvu’ kwani mchezo wa mpira wa miguu ni rahisi na wachezaji wake wako tayari kwa hilo.
 Bofya kumsikiliza.

No comments:

Post a Comment