KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, March 20, 2013

RAIS TENGA AIPONGEZA AZAM BAADA YA USHINDI WAKE DHIDI YA BARRACK YA LIBERIA.KOMBE LA SHIRIKISHO



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ameipongeza klabu ya Azam kwa ushindi wa mabao 2-1 ilioupata timu yake katika mechi ya raundi ya kwanza ya michuano ya Kombe la Shirikisho.
Mechi hiyo dhidi ya Barrack Young Controllers II ilichezwa jijini Monrovia, matokeo ambayo yanaweka Azam katika nafasi nzuri ya kusonga mbele baada ya mchezo wa marudiano utakaofanyika wikiendi ya Aprili 6 au 7 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
  Amesema Azam imefanya jambo kubwa, kwani kushinda ugenini hasa katika nchi za Afrika Magharibi si jambo dogo, hivyo Watanzania waendelee kuiunga mkono na anaitakia kila la kheri katika mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment