KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, March 26, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Reading yamwajiri Nigel Adkins kuchukua nafasi ya McDermott, Serikali ya Misri yaruhusu 10,000 kushudia mchezo dhidi ya Zimbabwe. TONY ANASEMA ALIMSHAURI PEP GUARDIAOLA KUJIUNGA MUNICH na McClaren awakumbusha na kuwausia vijana wa Roy Hodgson kuelekea mchezo dhidi ya Montenegro.

Klabu ya Reading ya nchini England imemtangaza bosi wa zamani wa Southampton Nigel Adkins kuwa meneja wake mpya.
Adkins, ambaye anachukua nafasi ya Brian McDermott, amesaini mkataba wa miaka mitatu na nusu ambao utamuweka ndani ya viunga vya Madejski mpaka kiangazi 2016.
Akiongea baada ya kusaini mkataba huo Adkins, ambaye atakuwa akisaidiwa na Andy Crosby, amesema kuwa Reading iko katika ligi kuu ya nchini England na kwamba kibarua chake ni kuhakikisha klabu hiyo inasalia katika ligi hiyo na kwamba amefurahishwa na kupata kazi hiyo.
Mtangulizi wake McDermott alitupiwa virago machi 11 na klabu hiyo baada ya kupata matokeo mabaya ya vichapo vinne mfululizo na kuiweka timu hiyo katika nafasi ya hatari ya kushuka daraja .

Mmiliki wa Readind Anton Zingarevich amenukuliwa akisema kuwa amefurahishwa na kumpata Nigel kwasababu anaamini ni chaguo sahihi kwa klabu hiyo.
Mtihani wake wa kwanza utakuwa ni Jumamosi hii dhidi ya Arsenal kabla ya kuungana tena na kikosi chake cha zamani Southampton Aprili 6 pale ambapo klabu hiyo itakapo ifuata Reading ukiwa ni mchezo ambao utakuwa ukiwakutanisha vibonde hao wa msimamo wa ligi ya England.
Serikali ya Misri yaruhusu 10,000 kushuhudia mchezo dhidi ya Zimbabwe.
 Takribani mshabiki elfu kumi nchini Misri wanajiopanga kuishangilia timu ya taifa ya Misri itakapo kuwa uwanjani kucheza dhidi ya timu ya taifa ya Zimbabwe Jumanne ijayo ukiwa ni mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia mwaka 2014.
Wizara ya mambo ya ndani ya Misri imetangaza kuruhusu idadi hiyo ya mashabiki kuingia uwanjani kuwashangilia Mafarao kwa mara ya kwanza ndani ya ardhi ya nchi hiyo, tangu kuwekwa kwa marufuku iliyotokana na maafa ya februari 2012 katika uwanja wa Port Said, ambapo jumla ya mashabiki 70 walipoteza maisha.

Vurugu hizo zilitokea wakati wa mchezo baina ya Al Masry na Al Ahly ambapo hivi karibuni hukumu ya kifo ilitolewa kwa  mashabiki kadhaa waliopatinaka na hatia ya kusababisha kuvugu hizo.

Misri inaamini kuwa uwepo wa mashabiki hao uwanjani kutaongeza hamasa ya kikosi chao cha timu ya taifa kuweza kufanya vizuri na hatimaye kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia mwaka 2014 zitakazo fanyika nchini Brazil na kurejesha nyuma kumbukumbu ya mafanikio yao ya mwaka 1990.

Ushindi dhidi ya Zimbabwe unatazamwa kama mwanzo mzuri kwa Misri kuingia raundi ya pili ya hatua ya mtoano kwani watatengeneza mwanya wa alama tano mbele ya Guinea, ambapo kinara pekee wa kundi atakuwa anasonga mbele kwenye hatua hiyo.

Zimbabwe itakuwa ikiongozwa kwa mara ya kwanza na kocha wa kijerumani Klaus-Dieter Pagels katika michezo ya kimashindano.

TONY ANASEMA ALIMSHAURI PEP GUARDIAOLA KUJIUNGA MUNICH.
Luca Toni ametanabaisha kuwa bosi mtarajiwa wa Bayern Munich Pep Guardiola amefanya naye mazungumzo kwa njia ya simu kabla ya kuanguka saini ya kuingia mkataba wa miaka mitatu na Bavarians.
Mshambuliaji huyo wa Fiorentina na kocha wa zamani wa Barcelona waliwahi kufanya kazi pamoja katika klabu ya Brescia kati ya mwaka 2001 na 2003 jambo ambalo limemfanya Guardiola kutokusita kuwasiliana na Toni na kuhitaji ushauri wake kabla ya kuelekea Allianz Arena.

Amenukuliwa Toni akisema,
"Alinipigia na kuniuliza kuwa ninaonaje hali ya Munich na jinsi nilivyokuwa nikiifahamu klabu hiyo wakati wa kipindi cha utumishi wangu"
"Bayern ni klabu safi sana. Maamuzi yake ya kuelekea Bayern yalikuwa sahihi kwake na klabu pia. Bayern kwasasa wana kocha bora na dunia kwa ujumla.
"Naamini kuwa Bayern itakuwa haishikiki Ulaya ndani ya muda mfupi"
Toni aliwahi kuvaa jezi ya Bayern kuanzia mwaka 2007 mpaka 2010, na kushinda taji moja la Bundesliga na moja la DFB-Pokal wakati wa utumishi wake ndani ya Munich.

McClaren awakumbusha na kuwausia vijana wa Roy Hodgson kuelekea mchezo dhidi ya Montenegro.
 Bosi wa zamani wa England Steve McClaren ameitaka timu ya taifa ya England maarufu kama ‘Three Lions’ kuonyesha kuwa wamejifunza kutokana na makosa ya miaka miwili iliyopita yaliyotokana na Wayne Rooney ambaye alionyshwa kadi nyekundu kuelekea kwenye mchezo dhidi ya Montenegro hii leo.

Mshambuliaji huyo wa Manchester United atakuwa akirejea uwanja wa Podgorica City kwa mara ya kwanza tangu alipokabidhiwa kadi hiyo alipokuwa katika dhamira ya kutaka kumfanyia kitu mbaya  Miodrag Dzuzdovic wakati timu hizo zilipokutana kwa mara ya mwishoni mwaka 2011.

McClaren amesema mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 na wenzake wanapaswa kuwa makini kujizuia na mazingira yatakayo kuwa yakiuuzunguka mchezo huo"

Ni kweli wanaweza kushinda mchezo huo bila wasiwasi lakini hili ni jaribio la uimara wao wa akili wa kupambana na mazingira ya nje ya uwanja wanapokuwa wanacheza na haya mataifa makubwa barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment