KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, October 25, 2013

UCHAGUZI BODI YA LIGI HAMAD YAHYA JUMA NDIO MWENYEKITI WA KWANZA

Hamad Yahya Juma wa Mtibwa Sugar ndiye Mwenyekiti wa kwanza wa Bodi ya Ligi Tanzania (Tanzania Professional League- TPL Board) baada ya kushinda katika uchaguzi uliofanyika leo mchana (Oktoba 25 mwaka huu) kwenye ukumbi wa mikutano uliopo Golden Jubilee Tower, Dar es Salaam.


Juma ambaye hakuwa na mpinzani alipata kura zote kumi za ndiyo zilizopigwa na klabu za Ligi Kuu zilizohudhuria mkutano huo. Klabu ambazo hazikuhudhuria uchaguzi huo ni JKT Ruvu, Mgambo Shooting, Coastal Union na Rhino Rangers.


Naye Said Muhammad Said Abeid ambaye pia hakuwa na mpinzani amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti kwa kupata kura zote za ndiyo.


Kwa upande wa wajumbe wawili wa Kamati ya Uendeshaji, wote Kazimoto Miraji Muzo wa Pamba na Khatib Omari Mwindadi wa Mwadui wameshinda kwa kura zilizopigwa na klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL).


Muzo alipata kura 15 za ndiyo wakati mbili zikimkataa, huku Mwindadi akipata kura 16 na moja ilimkataa. Klabu za FDL ambazo hazikuhudhuria uchaguzi huo ni Transit Camp, Burkina Faso, Polisi Mara, Stand United, Toto Africans, Polisi Tabora na Kanembwa JKT.

No comments:

Post a Comment