KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, February 3, 2014

Tennis: Nahodha wa tenis wa Ujerumani Carsten Arriens azomewa mashindanoni

Nahodha wa timu ya taifa ya mchezo wa tennis katika kombe la Davis, Carsten Arriens amezomewa na mashabiki wa nyumbani mjini Frankfurt jana Jumapili licha ya kuiongoza timu yake katika ushindi mnono wa 4-1 dhidi ya mabingwa mara tano wa kombe hilo Uhispania.
Sababu ya mashabiki kuchukua hatua hiyo ni kutokana na wachezaji maarufu wa tennis wa Ujerumani kujitoa katika kinyang'anyiro hicho kutokana na sababu mbali mbali.
Hii ilikuwa na maana kwamba mashabiki waliolipa kiasi cha euro 65 kuona mapambano ya wachezaji wawili wawili waliona pambano moja tu ambalo halikuwa na msisimko wowote, kati ya Daniel Brands na Roberto Bautista Agut wa Uhispania.

Michuano ya Olimpiki
Katika michuano ya Olimpiki ya Sochi, Rais wa kamati ya olimpiki ya Kimataifa IOC Thomas Bach amesema usalama wa kutosha na ukosoaji wa Urusi kuhusu sheria ya kupinga ushoga havitachafua michezo hiyo ya Olimpiki mjini Sochi.
IOC Kandidat Thomas Bach Mwenyekiti wa IOC Thomas Bach

Bach pia amerudia utetezi wake kuhusu matumizi ya fedha ya Urusi katika michezo hiyo , akisema kuwa fedha hizo zinakwenda katika kufanyia mageuzi ya muda mrefu katika eneo hilo. Akizungumza na waandishi habari siku nne kabla ya ufunguzi wa michezo hiyo, Bach ameeleza matumaini yake kwa uwezo wa Urusi kuweza kutoa ulinzi kwa michezo hiyo huku kukiwa na kitisho cha mashambulizi ya kigaidi kutoka kwa wapiganaji wa eneo la kaskazini mwa eneo la Kaukasus.

No comments:

Post a Comment