Carlo
Ancelotti anamatumaini kuwa Nene ataendelea kuwepo Paris Saint-Germain lakini
ni juu ya mchezaji huyo mwenyewe kuamua hatma yake.
Uwepo wa
winga huyo PSG upo mashakani tangu kuwasili kwa Ezequiel Lavezzi toka Napoli, na
Nene amekuwa akifikiria nini aamue kuhusu offer ya Corinthians.
Amenukuliwa Ancelotti
na Eurosport akisema
"ni juu
yake mwenyewe kuamua kama anataka kuondoka au anataka kusalia hapa kama atatuliza
akili atapata maamuzi.
"nimeongea
naye na klabu iko wazi tunachukua muda wetu kabla ya kuzungumzia juu ya
kuongeza muda wa mkataba wake.
"tutakuwa
wenye furaha kama ataamua kusalia kwa kuwa ni fantastic player na
anaweza kuwa muhimu katika msimu ujao."
Nene mwenye
umri wa miaka 31 alimaliza msimu katika ligi ya Ufaransa akiwa ni miongoni mwa
wafungaji bora akitupia nyavuni jumla ya mabao 21.Maktaba wake PSG utamalizika
kiangazi 2013.
No comments:
Post a Comment