Bosi wa Paris
Saint-Germain Carlo Ancelotti amethibitisha kuwa Zlatan Ibrahimovic atafanya
safari kuelekea Marekani jumanne
kujiunga na timu hiyo iliyoko katika ziara ya matayarisho ya msimu akiungana na
wenzake wapya katika timu hiyo.
Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa Sweden alikamilisha mipango yote ya uhamisho wake wenye
thamani ya euro milioni 23 akitokea AC Milan tangu July 18 ikiwa ni siku nne
baada ya mlinzi wa kibrazil Thiago Silva kufanya hivyo.
Mlinzi huyo
wa kati hajaelekea katika ziara ya Marekani kwa kuwa yuko katika kikosi cha Mano
Menezes ‘Selecao’ kinachojiandaa na Olympics lakini Ancelotti amesema Ibrahimovic
ataungana nao jumanne huku taarifa nyingine zikiarifu kuwa atakuwepo nchini
Ufaransa.
Kuelekea
kwenye msimu mpya kocha huyo wa zamani wa Milan ana matumaini kuwa mswedesh huyo ataisaidia sana timu yake.
Mchezo wa
kwanza wa kirafiki wa PSG ziarani Marekani utakuwa ni dhidi ya Chelsea utakao
pigwa jumapili.
No comments:
Post a Comment