Kocha wa Arsenal
Arsene Wenger anaamini kuwa ziara ya timu yake barani Asia itaongeza hari ya kikosi
chake wakati huu ambapo klbu hiyo imeshabariki kuondoka kwa nahodha wake Robin
van Persie.
Washika bunduki
hao wameelekea Kuala Lumpur kucheza na Malaysian XI na baadaye kuelekea Hong
Kong na Uchina kwa michezo mingine dhidi ya Manchester City na Kitchee SC.
Taarifa zinasema
Van Persie amegomea safari hiyo kwa lengo la kuongeza nguvu mipango ya uhamisho
wake kuelekea kwa mabingwa wa ligi kuu ya nchini uingereza.
Wenger pia
amezungumzia juu ya madhumuni mengine ya ziara hiyo ya barani Asia kuwa ni
kuungana na mashabiki wa soka timu hiyo ambao wako mashariki ya mbali.
No comments:
Post a Comment