Katika
michezo sita ya awali ya uzito wa Welterweight (69kg) ya michezo ya Olympic bondia
mzoefu na mwenye uwezo wa hali ya juu toka nchini Moldovan Vasilii Belous alikutana dhidi ya
mtanzania Selemani Kidunda.
Tangu
kupigwa kwa kengele bondia huyo alionekana kumfikia vilivyo bondia Mtanzania
Kidunda na kisha kuanza kufululiza straight
one-twos na hatimaye akamshinda Kidunda kwa points 20 kwa saba7.
Akiongea na
Rockersports toka nchini Uingereza kunako fanyika michezo hiyo ya Olympic, Kidunda
amesema kimsingi amekubali kushindwa lakini huo ni mchezo na kuna kushinda na
kushindwa hivyo mashabiki wake wasikate tama.
Hata hivyo
nilipomuuliza sababu za kushindwa na Vasilii Belous amesema kikubwa ni kwamba
mpinzani wake alikuwa akitumia mbinu chafu ya kumshika kila mara katika round
mbili za mwanzo jambo ambalo lilimfanya mwamuzi kumkanya kila mara hata hivyo
alifanikiwa kumdhibiti katika round ya tatu nay a mwisho.
Mchezo huo
ulikuwa ni wa round tatu na hivyo ukamalizika kwa Kidunda kupigwa kwa points 20
kwa 7.
Sasa Belous anasubiri
mzunguko wa pili dhidi ya bondia toka Ukraine Taras Shelestyuk.points 4 katika round
tatu alikuwa anaonyenywa
No comments:
Post a Comment