KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 30, 2012

KIMATAIFA:Meneja wa Arsenal Arsene Wenger: Giroud na Podolski hawatakuwa tayari kwa ajili ya msimu mpya na nyinginezo

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger: Giroud na Podolski hawatakuwa tayari kwa ajili ya msimu mpya.

Arsene Wenger amekiri kwamba maandalizi ya Arsenal kwa ajili ya msimu mpya hayajakwenda kama alivyopanga baada ya kudai kuwa Lukas Podolski na Olivier Giroud hawatakuwa tayari kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu ya kandanda ya England.
The Gunners wamemaliza ziara katika Bara la Asia kwa kucheza na mabingwa wa ligi kuu ya Hong Kong  Kitchee hapo jana na kutoka sare ya mabao 2-2 lakini mchezo wa kirafiki dhidi ya Nigeria uliokuwa umepangwa kufanyika mwishoni mwa juma umehairishwa na kuifanya sasa kusaliwa na mchezo mmoja tu dhidi ya Koln.
Mapema wiki hii Wenger ameweka wazi kwamba Jack Wilshere hatarejea hadi Octoba mwaka huu na kueleza kwamba wachezaji wake wengi huenda wasiwe tayari mwanzoni mwa msimu mpya wakiwa wamesalia majumbani kwao wakati wa ziara.
Amesema wachezaji ambao hawakuwepo katika ziara hiyo watahitaji michezo ya kutosha lakini baadhi watahitaji mchezo mmoja.

Tottenham inaamini Adebayor hatakamilisha mipango ya kurudi Manchester City

Tottenham bado inamatumaini ya kukamilisha mpango wa kumsaini kwa pauni milioni £5 mshambuliaji wa zamani wa Asernal Emmanuel Adebayor,licha ya mshambuliaji huyo kurejea katika mazoezi katika kikosi cha vijana cha  Manchester City jumatano.
Mazungumzo baina ya Adebayor na Spurs kwasasa yamekuwa yakiendelea na atakuwa akifanya mazoezi katika kituo cha mazoezi cha Manchester City cha Carrington wakati ambapo kikosi cha wakubwa kikiendelea na ziara ya Austria, Malaysia na China.
Spurs ilikuwa na matumaini ya kukamilisha uhamisho wa Adebayor wakati wakiwa zirani nchini Marekani mwishoni mwa wiki hii lakini hata hivyo mambo yanaonekana kwenda kinyume na matarajio.
Manchester City na Spurs zilifikia makubaliano wiki mbili zilizo pita kutoa ada ya pauni milioni £5 kwa ajili ya mchezaji huyo kufuatia kuwepo kwa mkopo muda mrefu White Hart Lane lakini Adebayor akikataa kutokana na kutoafikiana juu ya maslahi yake binafsi ndani ya klabu hiyo yenye maskani yake katika jiji la London.
Lakini hata hivyo kuna matumaini kuwa mpango huo utafanikiwa kutokana na utashi wa meneja mpya wa Spurs Andre Villas-Boas kutaka kujenga safu yake ya ushambuliaji lakini pia mwenyewe Adebayor kutaka mkataba wa kudumu ndani ya klabu hiyo.
Taarifa zinasema kuwa Adebayor amerejea kufanya mazoezi cha City akiwa na Roque Santa Cruz ambapo wamekuwa wakipata mshahara wa pauni £280,000 kwa wiki"
Imefahamika kuwa safari ya mshambuliaji huyo kuelekea White Hart Lane haitakamilishwa mpaka mapema mwezi ujao.
Adebayor alikuwa akiichezea Spurs akiwa mchezaji muhimu kwa mkopo msimu uliopita chini ya Harry Redknapp ambayo aliifungia jumla ya mabao 17 katika ligi kuu na kutoa pasi za mwisho zilizo zaa mabao 11 katika jumla ya michezo 33 aliyochezea timu hiyo.
Mshambuliaji huyo raia wa Togo alijiunga na City akitokea Asernal kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni  £25 mwaka 2009, lakini alijikuta akikosa nafasi katika kikosi cha kwanza baada ya mchezo dhidi ya Red Bull Salzburg mchezo wa michuano ya Europa December 2010.
  
Galliani: Matokeo ya hivi karibuni yamedhihirisha AC Milan kuendelea kuwa moto
Mkurugenzi wa AC Milan Adriano Galliani anaamini kuwa mchezo mzuri ulionyeshwa na timu yao katika michezo ya maandalizi ya kuanza kwa msimu imedhihirisha kuwa kocha  Massimiliano Allegri amekimiliki vema kikosi imara cha timu hiyo.
Kuuzwa kwa Zlatan Ibrahimovic na Thiago Silva kuelekea  Paris Saint-Germain, lakini pia kuwasili kwa mchezaji mwenye kiwango cha juu Riccardo Montolivo, kunaleta faraja na matumaini kuwa Rossoneri itatwaa taji.
Aidha Galliani ametoa maoni yake juu ya michezo ya wiki iliyopita ambapo walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya  Chelsea na Schalke kuwa imepigia mstari juu ya ubora wa Milan.

Baadhi ya mashabiki wa Milan bado wana matumaini kuwa klabu hiyo bado itakuwa na cheche zake licha ya kuacha wachezaji wao kadhaa waliokuwa nyota na wazoefu huku Galliani, akinukuliwa akisema timu hiyo kigogo nchini Italia kwasasa haina nafasi ya kufanya uwekezaji kwa wachezaji wenye majina makubwa.
Milan ambayo ilimaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Juventus msimu uliopita katika ligi ngumu ya Serie A inatarajia kuanza kampeni ya taji katika msimu mpya wa  2012-13 dhidi ya Sampdoria August 26.

No comments:

Post a Comment