Hatimaye Yanga imefanikiwa kutetea taji lake la michuano ya kombe la
Kagame baada ya kuifunga timu ngeni kwenye
mashindano hayo Azam, kwa mabao 2-0 mchezo uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka Uganda Hamis Kiiza alifunga bao la kwanza
dakika ya 44 na Said Bahanuzi akaongeza bao la pili ndani ya dakika za nyongeza.
Yanga wamezawadiwa dola 30,000, Azam wao wamepata dola 20,000 na Vita ya
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo walioifunga APR ya Rwanda 2-1 kwenye mchezo wa
kumtafuta mshindi wa tatu, wameondoka na dola 10,000.
Fedha hizo zimetolewa na Rais wa Rwanda Paul Kagame, ambaye ni mdhamini wa
michuano hiyo kwa miaka zaidi ya 10 na mashindano hayo yamepewa jina lake.
No comments:
Post a Comment