KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, August 31, 2012

KIMATAIFA:Mancini kunasa wanne kabla ya saa sita usiku huu na Allegri aambiwa waziwazi watu wanataka taji.


 Roberto Mancini ana matumaini kuwa Manchester City itakamilisha usajili wa wachezaji watani wenye thamani ya pauni milioni £40 kabla ya muda wa mwisho wa usajili kufungwa usiku wa leo.

Mancini anamfukuzia mlinzi wa kulia wa Inter Milan Maicon, mlinzi wa kati wa Fiorentina Matija Nastajic na kiungo wa Benfica Javi Garcia. Lakini pia anategemea kuwasajili Richard Wright na Scott Sinclair kuthibitishwa kama wachezaji wa City kwanza.

Sinclair amethaminishwa kwa pauni milioni £6.2, Maicon £4 na Garcia zaidi ya pauni milioni £20 wakati Nastajic amethaminishwa kwa pauni milioni £11 lakini City haitalipa pesa kamili kwasababu Stefan Savic anaelekea Italia kwa mpango wa kubadilishana.

Baada ya kuwa katika kipindi cha kuchekecha cha kiangazi City imefanikiwa kumsajili Jack Rodwell pekee ambapo kwasasa wanakamilisha biashara katika siku ya mwisho.

Amenukuliwa Mancini akisema
"endapo tutakamilisha mipango hii tutaimarisha timu yetu. Tunazungumza kuhusu mchezaji mmoja mkubwa unapomtaja Maicon, kwasababu anauzoefu na kijana Nastajic atakuwa mlinzi mzuri kwa muda mrefu."

Meneja huyo wa City anadhani Sinclair kama ni mbadala wa Adam Johnson aliyeuzwa lakini amesisitiza kuwa winga huyo wa Swansea hana uwezo wa kukokota mpira kama mchezaji mpya wa kutoka Sunderland.

"Sinclair anacheza nafasi moja kama Adam lakini tofauti ni kuwa Adam anatembea na mpira mguuni na Sinclair anatembea saba akiwa kwenye nafasi ".

City kesho itakuwa na kibarua dhidi ya QPR bila ya majeruhi kadhaa Gareth Barry, Micah Richards na Sergio Aguero.


Allegri aambiwa kavukavu 

 Massimiliano Allegri ameambiwa waziwazi kuwa yeye na vijana wake wanapaswa kupigania taji la Serie A kwa udi na uvumba hasa baada ya kuwasili kwa Nigel De Jong.

Kampeni ya msimu huu imeanza wakati ambapo Rossoneri ikiwapoteza wachezaji wake muhimu kama Zlatan Ibrahimovic na Thiago Silva. Wengine ni Alessandro Nesta, Clarence Seedorf na Pippo Inzaghi.

Baada ya kufungwa na Sampdoria, kumekuwepo na hali ya sintofahamu kiasi majaliwa ya hatma ya Allegri kumaliza msimu kuwa mashakani hasa ukifuatilia mahojiano ya Adriano Galliani aliyofanyiwa na La Gazzetta dello Sport.

Amenukuliwa makamu wa Rais wa Milan na Sports Daily akisema
"kwasasa Allegri hana sababu tena hapa Milan, shukrani kwa usajili wetu wa wachezaji wanne ambapo tutakuwa tunarejea katika mbio za kusaka  Scudetto.
“De Jong ni mmoja wa wachezaji wazuri na nguvu ulaya kwasasa anajua kazi na atatufanyia kazi”.

"tofauti kati yetu na wapinzani wetu sasa imepunguzwa Allegri hatakiwi kuficha hilo. Tunataka kucheza na kushinda taji si kumaliza katika nafasi ya tatu"

No comments:

Post a Comment