KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, August 1, 2012

Toa tongotongo kuhusu Mrisho Ngasa kwenda Simba.


Ngasa akikabidhiwa jezi ya Azam wakati akijunga nayo


Mrisho Ngasa mwenye mpira
 Habari zilizo zagaa hii leo juu ya usajili katika soka la Tanzania ni kuhusu kuingo wa Azam fc Mrisho Ngasa kuwa anaelekea kucheza soka msimu ujao wa ligi katika klabu ya Simba.
 Habari hizo zimethibitishwa na Viongozi wa Azam wenyewe kwa nyakati tofauti kupitia mahojiano ya simu na Rockersports kuwa kiungo huyo anapelekwa Simba kwa mkopo na Simba kutoa milioni 25 kunasa saini yake Ngasa ili aitumikie klabu hiyo kongwe hapa nchini.
Rockersports imefanya jitihada ya kufanya utafiti kwa kutumia vyanzo vikuu vinne juu ya taarifa hiyo ili kujiridhisha juu ya zoezi hilo la kukamilishwa kwa taratibi za uhamisho wa Ngasa kwa mkopo kunako klabu ya Simba.
Rockersports imeongea na pande zote mbili za mkataba huo yaani Simba na Azam, kisha ikaelekea upande wa kamati ya sheria, hadhi na wachezaji ya shirikisho la soka nchini TFF kujua hali ikoje inapotokea kuwepo na jambo kama hilo ambalo kimsingi muda wa kawaida wa usajili umeshamalizika na kipindi kinachoendelea ni cha kuidhinisha wachezaji wa mikopo.

Kama hiyo haitoshi Rockersports ikafanya mazungumzo na Ngasa mwenyewe juu ya hilo kupata ukweli hivi ni kweli anaelekea kucheza soka timu ya Simba?.
Ukweli wa mambo uko hivi, kwa utaratibu mchezaji kucheza soka katika timu yoyote ni makubaliano ya pande zote tatu, kwa maana ya timu anayotoka ,anayo kwenda na mchezaji mwenyewe jambo ambalo halikufanyika zaidi ya Simba kutangaza offer ya milioni shilingi 25 kwa ajili ya Ngasa na kukubaliana wenyewe bila ya saini ya mchezaji, je taratibu zimekamilika?
Pili katika makubaliano hayo kuna jambo la maslahi ya mchezaji ikiwemo mshahara na stahili nyingine kule anako elekea kucheza soka lazima kukubaliana jambo ambalo halikufikiwa.
Tatu ridhaa ya mchezaji mwenyewe kama timu anayo pelekwa inamfaa ama la, kwa Ngasa hilo anaonekana hayuko radhi nalo.
Azam watake wasitake Ngasa ni mchezaji wao ana mkataba na klabu yao, hivyo ni vema wakatumia busara kuliko hasira kwa yale yanayo fanywa na mchezaji huyo.

 Yapo mambo mengi ambayo tunayaona yakifanywa na Ngasa ambayo yana wakera viongozi wa Azam.
Mapenzi ya Ngasa kwa Yanga ni jambo la kawaida kwa mtu yoyote kupenda jambo au kitu fulani, huwezi kuzuia ni vema mkafuata taratibu za kumuuza kuliko kama ambavyo inavyoendelea sasa.

Akiongea na Rockersports Ngasa anasema hizo taarifa anazisikia tu lakini hajapewa taarifa rasmi na uongozi wa klabu yake na kama kuchezea Simba basi ni bora akae msimu mzima bila kucheza soka kwani thamani yake haijashuka kiasi kufikia milioni 25 wakati kuna timu zimetoa offer zaidi ya hiyo.
Namnukuu Ngasa
Simba ni timu nzuri kubwa na sina matatizo nayo,lakini, utaratibu huu sijaupenda, ningehusishwa na mimi katika mazungumzo yao lakini mimi sijui lolote nasikia tu
Kuna mengi nyuma ya pazia,
fikiria juu ya kauli yake hiyo.

Katika siku za hivi karibu hususani baada ya michezo ya kombe la Kagame kumeibuka hali ya sintofahamu hususani juu ya hatma ya Mrisho Ngasa ndani ya klabu yake ya Azam hasa baada ya mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka Yanga miaka miwili iliyopita, kubusu jezi ya Yanga na kushangilia bao la pili katika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, dhidi ya AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) akikimbilia upande wa mashabiki wa Yanga.

Kitendo kile kilizua hali ya sintofahamu ndani ya benchi la ufundi, viongozi na hata wamiliki wa klabu hiyo kwanini kafanya hivyo.
Sikatai kuwa linaweza kuvuruga utulivu wa akili ya mpenda soka, lakini sidhani kama linaweza kuifikisha klabu hiyo kufanya maamuzi ya kumuuza kwa style hii.
Ikumbukwe kuwa Ngassa amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake na Azam FC, akitokea Yanga miaka miwili iliyoipita kwa dau la Sh. Milioni 55.
Taarifa
Yanga imewasilisha offer ya shilingi milioni 50 Azam kutaka kumrejesha Ngasa Jangwani lakini Azam wanasema offer ya Yanga ilichelewa ndio maana wamekubali offer ya Simba ya milioni 25 , hivi kweli inaingia akilini wakati muda wa usajili wa wachezaji kwa mkopo haujafikia ukingoni kusema offer ya Yanga imechelewa?

1 comment: