KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, September 4, 2012

BAADA YA 'JABULANI' AFRIKA KUSINI , MPIRA UTAKAO TUMIA KOMBE LA DUNIA BRAZIL UMETAMBULISHWA 'BRAZUCA'


FIFA yataja jila la mpira wa kombe la dunia "Brazuca"
 
 
 Bodi ya utawala ya shirikisho la soka duniani FIFA imetangaza "Brazuca" kuwa ndio jina rasmi mpira utakao tumika katika fainali za kombe la dunia 2014.
Jina hilo limepigiwa kura na kupitishwa kwa asilimia 70% na kuizidi mipira ya Bossa Nova na Carnavalesca, hii ikiwa ni taarifa ya FIFA iliyotoka jumapili.
"Neno hilo hutumiwa na wabrazil kuelezea fahari ya maisha ya kibrazil. Wakielekeza hilo katika soka limeelezea kuwa hamu ,fahari na nia nzuri ".
Kwa mujibu wa katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke kura hizo zina maanisha kuwa kwa mara ya kwanza mashabiki wanajihusisha moja kwa moja na kutaja jina la mpira wa kombe la dunia.
Amenukuliwa akisema
"nina hakika kuwa mpira wa Brazuca utakuwa unaingia katika historia kama ilivyokuwa kwa mipira mingine ilikuwa na majina makubwa duniani kama ilivyokuwa kwa Tango nchini Argentina mwaka 1978 na Azteca nchini Mexico mwaka 1986,".
FIFA imesema mpira huo ulikuwa bado unaendelea kuimarishwa na kujaribiwa katika uzinduzi rasmi utakao fanyika kabla ya fainali za kombe la dunia 2014.

Zenit St Petersburg yamsajili Hulk na Witsel kwa pauni million  £64
 Mshambuliaji wa Kibrazil Brazil Hulk, ambaye alikuwa katika mazungumzo na Chelsea mwezi May, amejiunga na Zenit St Petersburg akitokea Porto kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £32.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ameingia mkataba wa miala miatano na mabingwa hao wa Russian, ambao wako chini ya meneja Luciano Spalletti.
Zenit pia imekamilisha kumsajili kiungo Axel Witsel, mwenye umri wa miaka 23, akitokea Benfica kwa ada kama hiyo.
Hulk amekaririwa akisema
"nilikuwa mwenye furaha Ureno na ninataka kuwa mwenye furaha hata hapa Russia pia."
Zenit St Petersburg iko katika jitihada za kuimarisha kikosi ambacho kinawinda akina Bruno Alves na Danny. Pia walikuwa wakihusishwa na kumtaka nyota wa Manchester United, Nani.
Witsel naye kama ilivyo kwa Hulk, naye ameingia mkataba wa miaka mitano.

Kocha muasisi nchini Misri Mahmoud el Gohary amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74
 Kocha mkongwe nchini Misri Mahmoud el Gohary amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74 baada ya kupatwa na ugonjwa wa kupooza ubongo akiwa Jordan.
Taarifa kupitia shirika la habari la MENA zimesema El Gohary anaangaliwa kama ni mtu muhimu na alama kubwa ya maendeleo ya soka nchini Misri ambapo aliwahi kuwa kocha wa timu ya Taifa ya nchini hiyo maarufu kama Mapharaoh katika fainali ya kombe la dunia mwaka 1990.
Katika fainali hizo mbali ya umaarufu mikubwa nchini kwake alipelekea timu yake kupata sare dhidi ya Uholanzi ya bao 1-1 yakiwa ni matokeo makubwa katika historia ya soka la nchi hiyo ikiwa ni pamoja na kuingoza Misri katika fainali za mataifa ya Afrika mwaka 1998 na kutwaa taji hilo.
Marekani  yaisimamisha  Falconets kombe la dunuia Wanawake FIFA U-20 
 Timu ya taifa ya wanawake ya Nigeria Falconets ya wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 imeshindwa kufikia fainali ya FIFA ya kombe la dunia ya U-20 kule Japan, baada ya kulambwa kwa mabao 2-0 kwa mabingwa mara mbili ya fainali hizo Marekani katika mchezo uliopigwa katika dimba la ‘Tokyo National Stadium’.
Mabao kupitia kwa Morgan Brian na Kealia Ohai yalitosha kuwaumiza wanigeria ambao katika fainali zilizo pita walikuwa washindi wa pili mika miwili iliyopita fainali zilizo fanyika nchini Ujerumani.
Falconets walitawala mchezo lakini walishindwa kutumia nafasi walizopata kwa kushindwa kupiga mashuti langoni mwa adui.
Sasa Marekani itakuwa inaingia katika mchezo wa fainali kwa mara ya tatu na watakuwa wakicheza dhidi ya ama Ujerumani au wenyeji Japan.
Mchezo wa fainali unatarajiwa kupigwa jumamosi katika uwanja wa taifa wa Tokyo National Stadium, baada ya mchezo wa kusaka mshindi wa tatu ambao Nigeria watacheza dhidi ya timu itakayo poteza katika mchezo kati ya Japan na Ujerumani.


No comments:

Post a Comment