KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, October 4, 2012

CRISTIANO RONALDO: MUHIMU KUJIAMINI KUELEKEA EL CLASICO NA MANCINI ANAKERWA NA UVIVU WA WACHEZAJI WAKE.


Cristiano Ronaldo, Kaka na Sergio Ramos wameelezea kufurahishwa kwao na ushindi wa Real Madrid wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Ajax na kusema kuwa wanaamini wataibuka na ushindi katika dimba la Camp Nou dhidi ya Barcelona katika mchezo ujao.
 
Ronaldo alikuwa shujaa wa kikosi cha Jose Mourinho akipiga ‘hat-trick’ wakati ambapo Ricaldo Kaka na Sergio Ramos wakianza katika mchezo licha ya kwamba hawakuwa katika kiwango kizuri.

Akiongea na kituo cha television cha Canal+, Ronaldo amenukuliwa akisema
"nimefurahi kwasababu tumeshinda na tumecheza vizuri, kwangu mimi kufunga magoli matatu na jambo kubwa.

"tumecheza soka letu kamili na ni jambo muhimu kuongeza kujiamini kuelekea katika mchezo ujao dhidi ya  Barcelona.

"ni muhimu kuondoka na mpira nyumbani lakini muhimu zaidi ni timu kwasababu bila wao nisingeweza kufunga magoli."
Barcelona inaweza kuongoza kwa kuongeza points 11 endapo itafanikiwa kuifunga Los Blancos katika mchezo wa jumapili, lakini Ronaldo anaamini kuwa kikosi chao kinaweza kuibuka na ushindi wanao utaka.

"nina matumaini kuwa tutapata matokeo mazuri katika eneo gumu la Camp Nou. Wana kikosi kizuri lakini hakutakuwa na utofauti mkubwa".

Wakati hayo yakiwa hivyo, licha ya kwamba amekuwa si chaguo la kocha lakini vilevile akiwa katika matatizo na kocha wake, Sergio Ramos hapo jana alianzishwa katika kikosi cha kwanza na amenukuliwa akisema anaamini wataendelea na mwendo wao mzuri.

"matatizo na Mourinho yamekwisha, na ninafuraha kwa ushindi katika mchezo wa ligi ya mabingwa, ushindi ambao ni muhimu katika timu".
"ulikuwa ni ushindi muhimu dhidi ya timu ngumu, lakini sasa tunaangalia mchezo wa La Liga.

"Clasico inakuja na siku zote ni ‘special’. Tunapaswa kuendelea na mwendo huu na kupata points zaidi katika ligi"

 ROBERTO MANCINI AKERWA NA UVIVU WA WACHEZAJI WAKE

 Roberto Mancini ameonya kuwa Manchester City inatakiwa kupigania kila mchezo kama wanataka kweli wanataka kushindana katika ligi ya mabingwa kauli ambayo ameitoa kufuatia kutapa sare ya bahati dhidi ya Borussia Dortmund.

Mabingwa hao wa ligi kuu ya England walikuwa katika kiwango kibovu katika sehemu kubwa ya mchezo wao dhidi ya mabingwa mara mbili wa Bundesliga , lakini hata hivyo wakafanikiwa kupata sare iliyotokana na mpira wa penati uliopigwa na Mario Balotelli na hivyo kuzima bao la utangulizi la Marco Reus.


Itakumbukwa City iliondolewa katika hatua ya makundi ya michuano hiyo msimu uliopita na sasa inaonekana kuwa katika hatari kama ya mwaka jana baada ya kuambulia point moja baada ya kushuka dimbani mara mbili.

Mancini ametupia lawama kikosi chake kwa kucheza soka bovu na kusema kikosi chake kimekosa kujituma na kukosa pia hamu ya ushindi na hiyo ndiyo sababu kubwa ya kucheza soka lisilo vutia.

Akinukuliwa na Sky Sports amesema,
"hatukucheza vizuri kwakuwa Borussia Dortmund walicheza vizuri kushinda sisi. Nadhani niwazuri zaidi kuliko sisi, kama tunataka tunataka kucheza katika kiwango cha juu cha ligi ya mabingwa ulaya, tunapaswa kukimbiza zaidi ya tulivyo fanya usiku huu.

"tunapaswa kukimbia, kupigania kila mpira. Sio tu kucheza pasi nzuri katika ligi ya ligi ya mabingwa ni zaidi ya hapo. Michuano hii ni ya kiwango kingine.

No comments:

Post a Comment