KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, November 21, 2012

Chelsea yajipanga kumtangaza mrithi wa Di Matteo


Imefahamika kuwa klabu ya Chelsea inajipanga kumtaja mrithi wa Roberto Di Matteo hii leo.

Di Matteo amefukuzwa kazi baada ya kichapo kichapo cha mabao 3-0 toka kibibi kizee cha Turin Juventus ukiwa ni mchezo wa michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.

Taarifa zinasema kuwa mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich amekuwa akimuhusudu Pep Guardiola lakini bado haijawa wazi endapo kocha huyo wa zamani wa Barcelona kama anaweza kurejea katika kazi hiyo ya ufundishaji.

Chelsea ilifanya mawasiliano na meneja wa zamani wa Liverpool Rafael Benitez kwa lengo la kumpa kazi ya muda mfupi.

Bodi ya Chelsea ilikutana mapema leo na huenda kazi ya mrithi wa Di Matteo ikatolewa kwa kipindi kifupi kifupi na si kazi ya muda mrefu kama ilivyokuwa kwa Di Matteo.

Katika taarifa iliyotolewa mapema asubuhi ya leo imesema Chelsea inataraji kumtangaza meneja wake mpya katika kipindi cha muda mfupi ujao.

Chelsea ambayo inasaka meneja wa tisa tangu klabu hiyo kununuliwa na Abramovich mwaka 2003, kabla ya mchezo wa jana ilikuwa imekwisha kufanya mawasiliano na Benitez akionekana kuwa ndiye chaguo sahihi.

Mameja walikuwa chini ya utawala wa Roman Abramovichni kama ifuatavyo,
    Claudio Ranieri: Sep 2000 to May 2004
    Jose Mourinho: Jun 2004 to Sep 2007
    Avram Grant: Sep 2007 to May 2008
    Luiz Felipe Scolari: Jul 2008 to Feb 2009
    Guus Hiddink: Feb 2009 to May 2009
    Carlo Ancelotti: Jun 2009 to May 2011
    Andre Villas-Boas: Jun 2011 to Mar 2012
    Roberto Di Matteo: Mar 2012 to Nov 2012.

Di Matteo ambaye alifanikiwa kushinda mataji ya klabu bingwa na msimu uliopita alikuwa katika kipindi cha utumishi cha miaka miwili kwa mujibu wa mkataba wake.

Bado mafao yake hayajafanyiwa kazi lakini vilevile ataendelea kulipwa mpaka hapo atakapo pata kazi sehemu nyingine.

Katika siku 262 za uongozi wake wa benchi la ufundi la Chelsea, Di Matteo anaonekana kama ndiye aliyekaaa kwa muda mrefu kuliko watangulizi wake Villas-Boas aliyedumu kwa siku 256, Avram Grant siku 247 na Luiz Felipe Scolari siku 223

No comments:

Post a Comment