KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, November 9, 2012

SIMBA YAWAANGUKIA MASHABIKI WAKE.

Klabu ya Simba ambayo ndio mabingwa watetezi wa taji la ligii kuu Tanzania Bara imewataka mashabikiwa wake kujitokeza hapo mkesho katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzani Bara kati yao na Toto Afrikans utakao fanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam klabu.

Simba imelazimika kuwaangukia mashabiki wao baada ya kuwepo tishio la mashabiki kugomea kwenda uwanjani kuwapa sapoti kufuatia timu hiyo kupata matokeo yasiyoridhisha katika michezo ya hivi karibuni.

Kauli iliyofanana na kuwabembeleza mashabiki hao imetolewa leo na msemaji wa klabu hiyo Ezekiel Kamwaga pale alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi.

Kamwaga ambaye mara kadhaa amekuwa akinukuliwa akitoa mifano ya yale yanayoltokea barani ulaya katika ligi kubwa za huko leo pia amendelea na mifano hiyo pale aliposema hata manchester United ilikaribia kutaka kushuka daraja lakini mashabiki wa vilabu hivyo vikubwa hawakuacha kuvihama vilabu vyao.

Mfano mwingine alioutoa Kamwaga ni kwamba  hata Liverpool ilishawahi kushukua daraja lakini mashabiki wake waliendelea kuisapoti jambo ambalo amelitaka mashabiki wa Simba kuiga mfano huo.

Amewata mashabiki hiyo kesho kujitokeza kwa wingi kwani endapo Yanga akatereza katika mchezo wa jumapili ni kwamba Simba itakuwa imemaliza mzunguko wa kwanza wakiwa wanaongoza ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment