KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, November 20, 2012

TAARIFA YA BFT YA KUSOGEZA MBELE MASHINDIANO YA NGUMI YA TAIFA




Mashindano ya klabu bingwa ya taifa 2012 yaliyokuwa yaanze Kufanyika kuanzia tarehe 26-30/11/2012 yamesogezwa mbele hadi 29/01-03/02/2013 kutokana na sababu mbalimbali.

Sababu zilizopelekea mashindano hayo kusogezwa mbele kubwa ni  hadi tunapotoa taarifa hii katika vyombo vya habari hakuna timu iliyokamilisha taratibu tulizoziweka za kuweza kusaidia kukamilisha mashindano hayo kwa ufanisi.

 Kwani katika barua ya taarifa ya mwaliko wa kushiriki katika mashindano BFT iliagiza kufikia tarehe 15/11/2012 timu zote ziwe zimethibitisha ushiriki wao ikiwa pamoja na kuwasilisha majina na picha za mabondia na viongozi watakaoshiriki  katika mashindano hayo na kulipa ada ya ushiriki ya Tsh. 200,000/=.

Hadi leo hakuna hata timu moja iliyokamilisha utaratibu huo kwa nia ya kupanga mashindano vizuri ili yawe na hadhi ya taifa kwa kuzingatia sheria za chama cha ngumi cha dunia (AIBA)
Sababu kama hizi mara nyingi zimesababisha mashindano mengi kuyaendesha katika kiwango cha chini na lawama nyingi kuelekezwa kwa BFT bila ya kufahamu sababu za msingi za kusababisha kutokea hivyo.kitu ambacho tungeweza kuepukana nacho kama tutafata taratibu tulizojiwekea. 

Kwani kwa kufanya hivyo tungejua mapema   idadi ya washiriki ili kupanga mipango halisi ya Kufanyika kwa mashindano.

Aidha kozi ya waamuzi iliyokuwa ianze tatehe 11-30/11/2012 imeshindwa Kufanyika kutokana na wanafunzi walikuwa wameomba kujiunga na kozi hiyo kushindwa kufika kwa wakati na kushindwa kukamilisha malipo ya kujiunga na kozi kwa wakati.

Kutokana na majukumu mengine  iliyonayo BFT kozi hiyo sasa itafanyika kuanzia tarehe 15/01-04/02/2013 na mazoezi ya vitendo yatafanyika katika mashindano ya klabu bingwa.
Kwa sasa BFT nguvu kubwa inaweka katika usajiri kwa makocha .waamuzi ,mabondia, madaktari katika data base za chama cha ngumi cha dunia (AIBA) ili wengi watambulike kwa ajili ya kujiunga na mashirikisho ya ngumi za kulipwa ndani ya ngumi za  ridhaa (AIBA PRO BOXING).


Makore Mashaga
KATIBU MKUU (BFT)

No comments:

Post a Comment