KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, December 31, 2012

UHAMISHO WA JANUARI ULAYA NDIO HUO SASA UMEWADIA. NANI ANAKWENDA WAPI NA NANI MWENYE KISU KIKALI. SNEIJDER, BEMBA BA, THEO WALCOTT, DAVID VILLA, MOROUANE FELLAINI, BALOTELLI, ZAHA, BENAT NA GOMIS WOTE SAFARINI.

Inavyo onekana mara baada ya dirisha dogo la usajili la mwezi Januari 2013 kufunguliwa mwezi January, hakutakuwa na uhaba wa upatikanaji wa vipaji.


Mwezi January sasa umefika ambapo dirisha dogo la usajili litakuwa likifunguliwa tena barani ulaya.  Kumekuwepo na majina mengi makubwa ambayo yamekuwa yakihusishwa na kutaka kuhama kutoka upande mmoja kuelekea upande mwingine, ambapo vilabu vikubwa katika bara hilo la Ulaya navyo vikihaha kusaka vipaji vipya.

Kwa msaada wa mtandao wa Goal.com hebu tuangalie majina hayo yanayotajwa kuwa huenda wakahama kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine mwezi huu wa January.

Wesley Sneijder, Inter
 Kiungo mchezeshaji huyo raia wa Uholanzi amekuwa hana nafasi tena katika kikosi cha kwanza San Siro. Sneijder ametamka waziwazi kuwa itakuwa vema kwake kama ataondoka katika klabu yake katika dirisha hili la usajili, kiasi kuviweka vilabu vikubwa barani humo kukaa mkao wa kumsubiri.

Taarifa za awali zinasema kuwa Sneijde ameshakubaliana katika mambo fulani ya msingi na klabu ya Tottenham na kwamba mpango huo umefikia hatua nzuri ambapo pia kuna vilabu kadhaa vya ligi kuu ya England vikimtamani kama vile Manchester City, Liverpool na Manchester United.

Pia Anzhi Makhachkala ya Russia pia iko katika mpango huo.

Demba Ba, Newcastle
 Mshambuliaji huyu ni raia wa Senegal ambaye amekuwa mfungaji mkubwa wa Newcastle, akiifungia magoli 29 katika jumla ya michezo 54 aliyocheza klabu hiyo.

Ba, amevutia vilabu vingi vikubwa ambapo Chelsea na Arsenal ni vilabu ambavyo kuna tetesi zinasema wanamtaka Ba mwenye umri wa miaka 27,

Kuondoka kwake kunaweza kumfanya meneja Alan Pardew kuwasajili Mathieu Debuchy na Loic Remy.


Theo Walcott, Arsenal
 Kwa hali ya mambo ilivyo ni kwamba mkataba wa Theo Walcott katika klabu yake ya Arsenal uko katika hali ya sintofahamu ambapo kwa kwasasa umekuwa unaangaliwa na vilabu vingi vikubwa barani Ulaya wakisubiri majaaliwa yake.

Wakati mkataba huo ukitarajiwa kumalizika mwisho wa msimu huu, vilabu mbalimbali sasa vimekodoa macho wakirubiri hatma yake mwezi January.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England mwishoni mwa juma alipiga bao tatu “hat trick” katika mchezo dhidi ya Newcastle ambayo kwa kweli imeongeza thamani yake katika mpango wake ujao usajili wa nyongeza kama washika mitutu watashawishika kumsajili tena Walcott na kwa vyovyote vile itakuwa ni busara kumsajili tena kuliko kumuacha akiondoka kama mchezaji huru majira ya kiangazi.

Kuna tetesi kuwa Chelsea na Manchester United wanamtaka nyota wa England, wakati ambapo Juventus na Paris Saint-Germain wakiwa mbioni kumnasa.

David Villa, Barcelona.
 Kama ilivyo kwa Sneijder, Villa pia ni jina kubwa ambaye amekosa nafasi ya kikosi cha kwanza katika klabu yake ya Barcelona lakini akionekana kuwa kivutio katika klabu kubwa za ligi kuu ya England “Premier League”

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 amekuwa katika kikosi kilicho anza cha Barcelona katika michezo 6 tu kati ya michezo 17 ambayo Barcelona imecheza ya ligi kuu ya Hispania ‘La Liga’ msimu huu ambapo sasa ameondoshwa rasmi katika orodha ya wachezaji wa kikosi cha kwanza moja kwa moja.

Meneja wa Chelsea Rafa Benitez inasemekana anataka kuwaunganisha wachezaji watatu wa timu ya taifa ya Hispania,Villa,Fernando Torres na Juan Mata katika kikosi chake, lakini Liverpool na Arsenal huenda wakaingia vitani kutaka saini yake. Pia huenda El Guaje akasalia Camp Nou kupigania nafasi msimu huu na kusubiri uhamisho wa majira ya kiangazi.


Marouane Fellaini, Everton

Nyota huyu raia wa Belgian alikuwa ni miongoni mwa wachezaji waliofanya vizuri msimu huu katika ligi kuu ya soka nchini England ‘Premier League’ anasifika kwa kipaji, akili na hata umbile la kisoka ikiwa ni pamoja na uwezo wa kumaliza mipira ya mwisho akitoa msaada mkubwa katika sehemu ya kiungo ya Everton maarufu  “Toffee”.

Fellaini alisaini mkataba wa miaka mitano mwaka uliopita lakini inasemekana anataka kuondoka Goodison Park, ambapo vilabu mbalimbali vikiwa vinataka huduma yake.

Real Madrid ni moja kati ya klabu kubwa inayo muawania mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye anasubiri kuona kama Everton itafuzu klabu bingwa Ulaya msimu huu na kuamua hatma yake.

  Mario Balotelli, Manchester City
 Baada ya kuwepo taarifa kwa muda mrefu kuwa huenda akaondoka katika klabu yake ya Manchester City, Super Mario Balotelli huenda akatimiza azma hiyo hivi karibuni  baada ya dirisha kufunguliwa.

Akiwa amefunga goli moja msimu huu, mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 22 uwanjani ameonekana kutokuwa na thamani hususani kutokana na kuzongwa na matatizo mengi ya nje ya uwanja.

Itategemea na taarifa ipi utakayo amini juu ya habari za Balotteli lakini ukweli ni kwamba meneja Roberto Mancini huenda akamuondosha kikosini ama akampa nafasi ya mwisho kutegemeana na vile anaona inafa.

Kutokana pia na City kuwa na azina kubwa ya washambuliaji, City huenda ikalazimika kukubali taarifa za tetezi kwamba Milan ilikuwa ikimtaka kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni could be forced to accept a rumored 20.


  Wilfried Zaha, Crystal Palace
 Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 amekuwa akivutia na kusisimua sana katika timu inayoshiriki ligi ndogo ya pili kwa ukubwa nchini England(Championship) ya Crystal Palace.

 Ana mambo mengi yan kuvutia ikiwemo nguvu na kipaji kiasi kupelekea kuitwa katika kikosi cha hivi karibuni cha timu ya taifa England.

Zaha ameonyesha wazi kutaka kuihama klabu yake mwezi januari ambapo tayari kuna klabu kama Liverpool, Arsenal, Manchester United, Tottenham, Chelsea na hata Real Madrid zikiwa zinamnyemelea na inaonekana wazi Palace haina ubavu wa kumzuia kiungo waliomsajili kwa pauni milioni 15.


Benat Etxeberria, Real Betis
 Kiungo huyu ana umri wa miaka 25 raia wa hispania amekuwa anacheza soka la kupendeza katika klabu ya Betis na kumekuwepo na taarifa za uwezekano mkubwa wa kuihama klabu yake mwezi huu wa januari dirisha litakapo funguliw.

Kiungo huyo wa zamani wa Bilbao hivi karibuni aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Hispania na kuna taarifa kuwa amekuwa akitakiwa na Barcelona.

Spartak Moscow na Wolfsburg pia zimetajwa kumuhitaji kama ilivyo kwa vilabu vya England ambavyo ni Tottenham, Liverpool Arsenal.


Bafetimbi Gomis, Lyon.
 Nyota wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa katika kiwango kizuri katika msimu huu akiifungia magoli 11 katika ligi kikosi cha Les Gones. Kwasasa klabu yake ya Lyon ya nchini Ufaransa imefulia kiunchumi na inalazimika kumuuza mlinda mlango wake nyota Hugo Lloris kwenda Tottenham majira ya kiangazi.

Gomis mwenye umri wa miaka 27 huenda akajiunga na Chelsea na Liverpool ambao wote wako mawindoni kumsaka mshambuliaji huyo aliyethaminishwa kwa pauni milioni 15.

No comments:

Post a Comment