KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, December 26, 2012

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Rafael Benitez anasema hao United na City wametangulia na baiskeli ya miti ngoja mwaka ugeuke, Mlinda mlango mzee Brad Friedel aanguka saini tena na Spurs, Mkongwe Del Piero ajitangazia mkataba mpya na Sydney FC na YAYA TOURE ANASEMA TAJI LA ENGLAND LITAKUWA GUMU KAMA MANCINI HATABADILI MBINU MPYA.



Meneja wa Chelsea Rafa Benitez anasema ana matumaini makubwa kuwa  Chelsea itarejea katika mbio za kuwania taji la ligi kuu ya nchin I England ‘Premier League’ baada ya mwaka mpya.

‘The Blues’ kwa sasa wako nyuma ya vinara wa ligi hiyo Manchester United kwa alama 11 licha ya kwamba wanamchezo mmoja mkononi ambao ulitokana na safari yao ya hivi karibuni nchini Japan ambako walikuwa wakishiriki michuano ya kombe la dunia la vilabu.

Baada ya ushindi wa kutakata wa mabao 8-0 dhidi ya Aston Villa jumapili iliyopita, Chelsea sasa inajipanga na michezo mitatu dhidi ya Norwich, Everton na Queens Park Rangers michezo ambayo itachezwa kabla ya januari 2, ambapo Benitez anaimani timu kupitia michezo hiyo itafanikiwa kuwasogelea vinara Manchester United na Manchester City walioko kileleni katika msimamo wa ligi.

Alipoulizwa kama alishawahi kuwaambia wachezaji wake kuwa bado wanayo nafasi ya kutwaa taji hilo, Benitezi amesema

"tutaliaona hilo baada ya michezo miwili mpaka mitatu ijayo na utashuhudia hali ya kujiamini ikijengeka miongoni mwao na hiyo ndio hatma ya yote”

"wana tembea vizuri uwanjani, wanatengeneza nafasi sasa tunapaswa kuendeleza mwendo huo na itakuwa rahisi kwangu kusema tunaweza kushindana".

Benitez aliajiriwa kama meneja wa muda baada ya kufukuzwa kazi mtangilizi wake Roberto Di Matteo mwezi November ambapo alikutana na upinzani mkubwa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo lakini alitulia na kuongeza nguvu kwa wachezaji wake tangu alipowasili.

Juu ya hilo amesema

"wachezaji walikuwa makini tangu siku ya kwanza, walijua kuwa wanameneja mpya na wanatakiwa kucheza soka na tangu siku hiyo walijitahidi kujifunza na kuongeza juhudi na wamekuwa wakifanya hivyo"

Mlinzi wa Chelsea Gary Cahill anaamini Benitez sasa ameanza kupata ushindi dhidi ya wapinzani wake baada ya kuonyesha soka dhidi ya Aston Villa.



Yaya Toure ataka Man City kubadili mbinu kama si hivyo.....
 Yaya Toure amesisitiza kuwa Manchester City inapashwa kuwa ikibadilika mara kwa mara katika mbinu zake za uchezaji kama wanataka kweli kulichukua tena taji la ligi kuu ya England walilotwaa msimu uliopita.

Toure, ambaye alikuwa msaada mkubwa katika harakati za kutwaa taji hilo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 44 kupita, anaamini wapinzani wao wanazijua mbinu zao na wanatumia namna mbadala ya kutengua mbinu hizo  za kiuchezaji na kuharibu mapeni yao.

Kuelekea kwenye mchezo wa leo ndani ya siku ya Boxing Day dhidi ya Sunderland, Toure anasisitiza juu ya nia yake ya kumuona meneja Roberto Mancini ili kuangalia namna ya kubadili mbinu kuendelea ushindi na kupata magoli zaidi.

Akiongea na gazeti la the Sun amekaririwa akisema,

"msimu huu tunashindwa kucheza ukilinganisha na msimu uliopota kwakuwa wapinzani wetu wanajua jinsi tunavyocheza".


"wakati meingine tunapaswa kubadilisha mfumo wetu ili kuzisimamisha hizi timu, timu nyingine na wachezaji wao wanatambua jinsi tunavyocheza, wanatusoma na wanafanyia kazi kutusimamisha. Hata zile timu zilizo chini katika msimamo wa ligi wanatupa shida.

"timu ambayo tuliifunga goli 4-0 msimu uliopita wamejifunza mfumo wetu wa uchezaji na wamebadili mbinu ya kukabiliana na sisi. Hawataki kufungwa magoli mengi tena.

Kwasasa Manchester City iko nyuma kwa alama nne kwa vinara Manchester United.


Rooney anasema kiwango kitarejea katika mchezo dhid ya Toon

Baada ya kuonekana kama vile sasa anakwisha na kufunikwa na Robie van Persie, mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney amesema moto wake  utarejea kama kawida katika mchezo dhidi ya Newcastle United.

Rooney hakufua dafu jumapili katika mchezo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1 kule Liberty Stadium, ambapo hakuwa vizuri, akipoteza mipira mingi na kukosa magoli. 

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England anasema mchezo wa sikukuu ya leo ni nafasi tosha kurejesha heshima yake mbele ya mashabiki wake na wa United kwa ujumla akianza na mchezo wa leo mbele ya wageni Newcastle katika dimba la Trafford.


Baada ya kugundua umri unamuacha, Del Piero ajitangazia mkataba mpya na klabu yake ya Sydney FC.
  Alessandro Del Piero amedokeza kuwa anatarajia kuongeza mkataba wake na klabu ya Sydney FC inayocheza  ligi kuu ya nchini Australia A-League na kusema kuwa lengo lake katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka ni kuhakikisha Sydney FC, inapanda katika usukani wa ligi hiyo.

Del Piero na wachezaji wenzake wa timu hiyo wanahaha kuiondosha timu yao kutoka katika nafasi ya chini ya msimamo wa ligi hiyo wakati huu ambapo wanaelekea katika mchezo mgumu na wapinzani wao wakubwa wa jiji la Sydney Central Coast Mariners mchezo utakaopigwa hapo kesho alhamisi.

Del Piero mwenye umri wa miaka 38 bado hajafikia makubaliano na klabu yake ya kumuongezea mkataba mwingine , lakini mwenyewe anaamini malengo yake ni kuendelea kusalia Sydney.

 Licha ya uzee wake, Brad Friedel amaliza uvumi wa kuelekea Blackburn asaini tena na Tottenham.
 Brad Friedel amesaini mkataba mpya na klabu yake ya Tottenham.

Mlinda mlango huyo ambaye mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika baada ya kumalizika msimu huu wa ligi, tayari amesha kubaliana na klabu yake na kusaini mkataba mwingine wa nyongeza wa mwaka mmoja kusalia ndani ya klabu hiyo mpaka kiangazi 2014.

Friedel atakuwa anakamilisha miaka 43 ya kuzaliwa kwake baada ya mkataba wa mpya kumalizika na anajipanga kuhakikisha anakuwa mlinda mlango nambari moja wa klabu hiyo kama alivyokuwa akidhani kupata timu ya kucheza kikosi cha kwanza baada ya mkataba wake kumalizika huko Hugo Lloris.

Spurs imetangaza kumuongeza mkataba mlinda mlango huyo na kuwamaliza kabisa Blackburn ambao walikuwa wakimtolea macho mkongwe huyo kwa lengo la kumrejesha Ewood Park.

No comments:

Post a Comment