KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, January 12, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Furguson anasema Suarez anapenda kuzongwa na maneno. Rafael Bernitez amtetea mchovu Torrez. Mancini hana jinsi lazima amsajili Tevez. Steven Gerrard apinga sera za Brendan Rogers na alikatazwa na marehemu mama yake kupiga penati.

 Ferguson: Suarez anapenda kuzongwa zongwa.
Kuelekea katika mchezo wa kesho dhidi ya Liverpool hapo kesho, meneja wa mashetani wekundu Sir Alex Ferguson anaamini Luis Suarez ni mtu ambaye anapenda kuzingirwa na mizozo.
Suarez atakuwa akiikabili United katika uwanja wa Old Trafford hapo kesho kwa mara ya kwanza tangu alipogomea kupenea mkono na Patrice Evra mwezi February mwaka jana.

 Tukio hilo ni moja kati ya mlolongo wa matukia yanayo muhusu mshambuliaji huyo ambayo yamekuwa yakiibua gumzo kubwa.

Mruguay huyo kwa mara nyingine aliingia katika mjadala wiki hii pale alipofunga goli dhidi Mansfield mchezo wa michuano ya FA goli ambalo lilithibitika wazi kuwa kabla ya kufunga alitumia mkono kuutengeneza mpira kabla ya kupiga kwa mguu wake wa kulia na kutumbukiza wavuni.

Sir Alex Ferguson anadai kuwa hakushangazwa na Suarez kuingia katika gumzo lingine kubwa kama hilo.
Amenukuliwa akisema
"Sikuangalia mchezo dhidi ya Mansfield, hivyo ni vigumu kusema kama ilikuwa ni makusudi ama hapana".
"lakini nadhani huyu kijana amekuwa ni mtu wa kuzongwa zongwa sasa sijui kama anafurahia hiyo au laa."

Benitez amtetea Torres.
 Rafael Benitez amemtetea mshambuliaji wake Fernando Torres wakati ambapo kumejitokeza ukosoaji mkubwa kwa mshambuliaji huyo raia wa Hispania na anaamini kuwa mshambuliaji huyo atafanikiwa kuwashinda mashabiki wakosoaji wake wa klabu yake ya Chelsea.

Torres mwenye umri wa miaka 28, ameifungia Chelsea magoli 14 msimu huu lakini kiwango kibovu katika mchezo dhidi ya Swansea mchezo wa michuano ya Capital One kimeibua maswali mengi juu ya nafasi yake katika timu.

Kuongezwa kwa Demba Ba kikosini ambaye alifunga magoli mawili kati ya matano katika mchezo wa michuano ya FA dhidi ya Southampton ambapo Chelsea ilishinda 5-1 kumeibua shinikizo jipya kwa mshambuliaji wengi wakitaka akazane zaidi, lakini hata hivyo Benitez amemtetea Torres kwa kusema kuwa alikuwa anaumwa siku ya mchezo dhidi ya Swansea.

Mancini anamatumaini ya kumsajili tena Tevez.
 Roberto Mancini amesema anatarajia klabu yake ya Manchester City itampa mktaba mpya  mshambuliaji muargentina Carlos Tevez.
Mkataba wa sasa wa Tevez utamalizika katika kipindi cha kiangazi mwaka 2014.
Kwasasa City haiko tayari kumpoteza mchezaji ambaye aliwagharimu ada ya uhamisho ya pauni milioni £25 ndani ya kipindi cha miezi 18.

Hali hiyo moja kwa moja itamzuia Roberto Mancini kupata mchezaji mbadala yake kwani sheria ya udhibiti wa matumizi ya shirikisho la soka Ulaya EUFA zinawazuia kufanya hivyo kwakuwa wanatakiwa kuweka sawa mzani wao wa matumizi katika vitabu vyao na kwamba wanatakiwa kuuza kabla ya kununua.

Hiyo pia inaangaliwa kama ni ujenzi mpya wa mahusiano mazuri baina yao, tangu kipindi kile ambacho Tevez alipogomea kufanya mazoezi ya kupasha misuli moto kabla ya kuingizwa uwanjani katika mchezo wa michuano ya klabu bingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich mwezi September 2011 ambapo alikaririwa Manchini akisema mchezaji huyo amejimaliza.

Hali hiyo ilipelekea Tevez kupoteza pauni milioni £9.3 kama makato yaliyotokana na sehemu ya mshahara wake na bonasi nyingine sambamba na kukalia benchi kwa miezi sita kabla ya kurudi na kuisaidia City kushinda taji la ligi kuu ya England.

Steven Gerrard apinga sera ya meneja wake.
  Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard ameonya mpango wa meneja wake Brendan Rodgers wa kutaka kuwatumainia zaidi vijana katika kipindi cha mapinduzi makubwa ya Anfield.

Tangu kuwasili kwa Rodgers kiangazi mwaka jana, wekundu hao wamekuwa na mpango wa kuwasajili zaidi wachezaji vijana na tayari imefanya hivyo kwa Joe Allen, Fabio Borini na Daniel Sturridge ambao wote bhawajafika umri wa miaka 24.

Steven Gerrard na McAllister mwaka 2000.
Gerrard ambaye kwasasa ana umri wa miaka 34, hana imani kama sera hiyo kama itaivusha Liverpool kuelekea kwenye mageuzi yanayotakiwa hivi sasa, ikiwa kwasasa iko katika nafasi ya nane katika msimamo wa ligi ya ‘Barclays Premier’ hivyo ni vigumu kwa sera hiyo kuirejesha katika changamoto ya michuano mikubwa ya vilabu ulaya kama klabu bingwa.

Kiungo huyo ametolea mfano usajili wa Gary McAllister ambaye alisajiliwa Anfield akiwa na umri wa miaka 35 mwaka 2000 kuwa ulikuwa ni mpango wa maendeleo na kwamba itakuwa vizuri kama kutakuwa na mchanganyiko wa umri katika kikosi.
Amenukuliwa akisema,
'Sikubaliani na sera hiyo kiukweli'.
'nimeona usajili mwingi duniani kote watu wanasajili umri wa miaka 28, 29na pengine zaidi ya hapo na wanafanya kazi nzuri kwa kweli. Sitaweza kuielewa sera hii japokuwa ni kweli kila mtu anataka wachezaji vijana wenye akili Waingereza lakini si kwa asilimia 100.

 Kuelekea fainali za mataifa ya Afrika 2013
Asamoah Gyan anasema ni usia wa mama yake asipige tena penati katika timu ya taifa.
Nahodha wa timu ya taifa ya Ghana Asamoah Gyan ameweka wazi msimamo wake kuwa hayuko tayari kupiga penati katika muda muda wa kawaida katika michezo ya mataifa ya Afrika inayotarajiwa kuanza nchini Afrika Kusini januari 19.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alikosa penati ambayo pengine ingeipeleka Ghana kwenye husu fainali ya kombe la dunia mwaka 2010 na katika nusu fainali ya michuano ya mataifa ya Afrika mwaka jana.

Baada ya kupata usumbufu mkubwa wa matusi na mengine akitukaniwa mama yake kutoka kwa mashabiki, matusi ambayo yalimfanya apumzike kuichezea timu ya taifa , Gyan amerejea huku akitoa tamko la wazi kabisa kuwa hatapiga mpira wowote wa penati katika fainali hizi.
Amenukuliwa akisema
"nimeamua kutokupiga penati katika timu ya taifa".
"wachezaji wengi wakubwa wamekosa penati Cristiano Ronaldo, Lionel Messi, Diego Maradona wote wachezaji wakubwa na katika siku mbaya inaweza kutokea.
"lakini kama nilivyosema mwezi uliopita sitapiga tena penati. Kabla mama yangu hajafa mwezi November aliniambia nisipige tena penati."

No comments:

Post a Comment