KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, March 29, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Nahodha wa Fulham Hangeland aongeza mkataba. Bixente Lizarazu amzodoa David Beckham.YOHAN CABAYE ANASEMA MAN CITY HAICHEZI KITIMU KAMA UNITED. MANCINI AKERWA NA KOMPANY. CHAMA CHA SOKA ENGLAND CHAMTOSA RIO FERDNAND KUBAGULIWA na NIGERIA WATAKA MAREKEBISHO YA RATIBA YA KOMBE LA DUNIA. .

Nahodha wa Fulham Brede Hangeland aongeza mkataba.
Nahodha wa wa timu ya Fulham Brede Hangeland ameongeza mkataba wa miaka miwili wa kusalia katika viunga vya Craven Cottage mpaka mwaka 2015.
Mlinzi huyo raia wa Norway makataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu ambapo sasa ameamua kusali hapo kwa miaka mingine miwili
Hangeland mwenye umri wa miaka 31, alijiunga na Fulham akitokea FC Copenhagen mwezi January 2008 kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 2.5, na ameitumikia klabu hiyo ya London ya magharibi kwa zaidi ya michezo mia mbili.
 Amekaririwa akisema kuwa amekuwa ni mwenye furaha katika kipindi chote alichokuwepo ndani ya klabu hiyo.

Bixente Lizarazu amzodoa David Beckham.
 Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa Bixente Lizarazu anadhani kuwa kuwa kiungo wa Paris Saint-Germain David Beckham alikosa uweledi lipofanya ziara ya kuitembelea china siku chache tu kabla ya mchezo wa kwanza wa robo fainali dhidi ya Barcelona.
Beckham alizuru mashariki ya kati wakati wa mapumziko ya michezo ya kimataifa akiwa kama balozi wa China, ambapo Lizarazu anadhani kiungo huyo wa zamani wa Manchester United alipaswa kuwa katika maandalizi ya mchezo dhidi ya Barca.
Akiongea na TF1, Lizarazu amesema katika hilo hawezi kumuunga mkono Beckham kwa kufanya ziara siku kumi kabla ya mchezo muhimu wa msimu, na kwamba jambo hilo halikuwa sahihi.
Beckham ameitumia PSG jumla ya michezo mitano tu, tangu ajiunge nayo katika msimu wa usajili wa dirisha dogo la mwezi January.

YOHAN CABAYE ANASEMA MAN CITY HAICHEZI KITIMU KAMA UNITED
 Kiungo wa Newcastle Yohan Cabaye anaamini kuwa Manchester City haichezi kitimu na hiyo ndiyo sababu kubwa inayoigharimu timu hiyo.
Kikosi cha meneja Roberto Mancini tayari kinaonekana kupoteza matumaini ya kutetea taji taji wakati huu ambapo wako nyuma kwa vinara wa ligi hiyo Manchester United walio mbele yao kwa mwanya wa alama 15 kileleni.
Kuelekea kwenye mchezo wa Newcastle dhidi ya City, kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 amedai kuwa kikosi hicho kimesheheni wachezaji wazuri lakini hakifanyi kazi kwa umoja.
Amenukuliwa na gazeti la The Sun akisema
"United ni mashine na kwamba Sir Alex anafanya kazi nzuri katika klabu yake, hata kama wachezaji wanabadilika kwakuwa anajua ni mchezaji gani atakuwa mzuri katika timu.
“City wanawachezaji wazuri lakini bahati mbaya kwao hawachezi kama timu si kama United"
Cabaye alikuwa akikabiliana na wakali wa Hispania Xavi, Andres Iniesta na Sergio Busquets wakati wa mchezo wa kimataifa mchezo ambao Ufaransa walipoteza kwa bao 1-0.
Anatarajiwa kuchukua sehemu ya kiungo akipambana na Yahya Toure jumamosi pale ambapo Newcastle watakapokuwa wakipambana dhidi ya Manchester City.

MANCINI AKERWA NA KOMPANY.
 Bosi wa Manchester City Roberto Mancini amemtaka mlinzi wake wa kati Vincent Kompany kuweka kwanza kipaumbele katika majukumu ya klabu yaike kuliko kuiwakilisha Belgium.
Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka26 aliitwa na kocha Marc Wilmots kuunda kikosi cha Belgium kwa ajili ya majukumu ya kimataifa wakati wa mapumziko ya michezo ya kimataifa huku akikosekana katika timu yake tangu mwezi Januari.
Mchango wa Kompany uliisaidia Belgium kuibuka na ushindi wa bao 1-0 na mlinzi huyo akicheza dakika zote 90 za mchezo mjini Brussels jumanne jambo ambalo limemuhuzunisha Mancini.
Akinukuliwa Mancini akiongea na The Manchester Evening akisema
"Wakati mwingine mchezaji anatakiwa kuelewa kuwa klabu yake ni muhimu zaidi na wala si semi kuwa timu ya taifa si muhimu na sitawaambia wachezaji wangu kuwa wasicheze katika mataifa yao"
"hajaichezea timu yake kwa siku 60 lakini amekwenda kuichezea timu ya taifa ya Belgian, Sikubaliani na hilo. Wakati mwingine mameneja wa timu za taifa wanapaswa kuelewa hali ilivyo, hawa wachezaji wanavilabu vyao na wanalipwa mishahara kila mwezi”.

CHAMA CHA SOKA ENGLAND CHAMTOSA RIO FERDNAND KUBAGULIWA.
 Chama cha nchini England FA kimesema kuwa kimekosa ushahidi wa kwamba mashabiki wa soka wa chini hiyo waliimba wimbo za kumbagua mlinzi wa Manchester United Rio Ferdinand na ndugu yake mlinzi wa QPR Anton, wakati wa mchezo baina ya England maamrufu kama ‘Three Lions' dhidi ya San Marino.
Katika taarifa iliyotolewa mkurugenzi wa vilabu ndani ya FA Adrian Bevington imesema kuwa
"Ndani ya San Marino, tulikuwa na wakuu wa usalama wa FA waliokuwa wakifuatilia mashabiki wa England ndani ya uwanja , na hiyo inajumuisha rikodi za video tulizo zifuatilia.”

NIGERIA WATAKA MAREKEBISHO YA RATIBA YA KOMBE LA DUNIA.
 
 Nigeria wanataka ratiba ya kombe la dunia kurekebishwa.
Shirikisho la soka nchini Nigeria NFF limelitaka shirikisho la soka duniani FIFA kurekebisha ratiba ya michezo ya timu ya taifa ya nchi hiyo ‘Super eagles’ ya mwezi june kwa lengo la kutaka haki kutendeka huku wakitaka michezo yote ya kundi F ifanyike siku.
Wiki iliyopita Fifa ilirekebisha tarehe za michezo ya Super Eagles kufuatia Nigeria kukabiliwa na michezo mingine ya michuano ya kombe la shirikisho la dunia mwezi June.
Nigeria itacheza na Kenya jijini Nairobi Juni 5 kabla ya kusafiri kuifuata Namibia wiko moja baadaye na pia kuelekea nchini Brazil Brazil kwa ajili ya michezo ya michuano ya shirikisho
Michuano hiyo ya shirikisho ambayo itajumuisha mataifa ya Hispania ambao ndio mabingwa wa dunia pamoja na mataifa bingwa kutoka mabara sita itakuwa ikifanyika nchini Brazil kuanzia juni 15.
Michezo ya kufuzu ya hatua ya makundi ndani ya mwezi juni huenda ikafanyika kati ya 5 na 12 ama tarehe zilizokuwa zimepangwa hapo awali juni 8 na 15.
Nigeria wanaongoza kundi hilo wakiwa wanakabana koo na Malawi wakitofautiana kwa magoli ya kufunga na kufungwa na wote wakiwa na alama tano baada ya michezo mitatu.
Katibu mkuu wa NFF Musa Amadu ameelezea sababu ya shirikisho hilo kupeleka ombi lao Fifa akisema lengo kutafuta haki na kuzuia upangaji wa matokeo.

No comments:

Post a Comment