Shirikisho
la soka barani Ulaya EUFA limesema limegundua
kujitokeza kwa vitendo vya kibaguzi kwa baadhi ya wachezaji na maafisa kadhaa sasa huneda wakakabiliwa na kifungo cha michezo 10 ikiwa ni
sehemu ya mpango mpya uliopendekezwa na EUFA.
Katibu mkuu
wa shirikisho hilo Gianni Infantino amesema vilabu vitakavyogundulika na tuhuma
hizo huenda vikalazimika kufunga sehemu ya uwanja wao ambazo mashabiki wao
wamekuwa wakifanya vitendo hivyo.
Kumekuwepo
na gumzo kubwa juu ya vitendo vya aina hiyo ambavyo vimekuwa vikijitokeza msimu
huu hususani baada ya kiungo wa AC Milan Kevin-Prince Boateng kuongoza baadhi
wa wachezaji wenzake kutoka uwanjani katika mchezo mmoja wa kirafiki nchini
Italia.
Raia huyo wa
Ghana aliondoka uwanjani katika mchezo dhidi ya Pro Patria baada ya kusikika
maneno ya kibaguzi kutoka kwa mashabiki.
Akiongea katika mkutano wa Soccerex Global Convention 2013 jijini Manchester hii leo Infantino amesema kuwa mkutano huo ni mkubwa wa kibiashara katika soka ambaopo amenukuliwa akisema.
"Ina maana kuwa sehemu ambayo itapatikana na hatia ya kurusha maneno ya kibaguzi itafungwa pamoja kupigwa faini ya euro 50,000 (£42,700)"
Huko nyuma
nahodha wa Chelsea John Terry na mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez waliiingia
matatizoni baada ya kukumbana na kashfa ya kutumia lugha za kibaguzi.
Mwezi Mei
kamati ya utendaji ya Uefa inatarajiwa kupigia kura mapendekezo hayo jijini London
na huenda sheria hiyo ikaanza kutumika katika michuano ya Uefa kuanzia mapema
mwezi Julai.
Mkutano wa November 23 mpaka 27/ 2013 utakuwa unakamilisha sehemu ya mwisho ya mkutano wa Soccerex
Global Convention ambao utafanyika Rio de Janeiro.
Mkutano huu
ni flagship ambayo inakutanisha maamuzi makubwa ya kisoka ambapo zaidi ya wajumbe 4,500
wanakutana kwa siku tano za kufahamina, kujifunza na kuzungumza biashara.
Mkutano wa Rio
utakuwa unaweka mipango ya miaka minne ijayo katika eneo la maendeleo ya
biashara ya soka, kabla ya kombe la dunia
la FIFA 2014 na michuanio ya Olympic 2016 kabla ya kuangalia fursa mbalimbali
kuelekea michuano hiyo mikubwa.
Equatorial guinea huenda ikapoteza
ushindi wao dhidi ya cepe verde
![]() |
Timu ya taifa ya Equitorial Guinea kufungiwa kwa kutumia wachezaji si wazawa. |
Equatorial
Guinea huenda ikavuliwa ushindi wao wa bao 4-3 dhidi ya Cape Verde mchezo wa kufuzu
kombe la dunia 2014, kufuatia kumchezesha mchezaji ambaye hakuwa halali kutumiwa na
timu hiyo.
Fifa imesema
imefungua kesi dhidi ya chama cha soka cha Equatorial Guinea FA baada ya
ushindi wao wa mwezi uliopita uliofanyika mjini Malabo kufuatia kutuhumiwa na
Cape Verde.
Bodi ya
utawala ya FIFA imesema bado haijathibitisha juu ya tuhuma hizo na kwamba bado
wanaendelea na uchunguzi.
Kwa mujibu
wa kifungu nambari cha 17 cha katiba ya FIFA kinasema kuwa ili mchezaji kuwa
halali kutumikia timu ya taifa anapaswa kuwa mzaliwa wa taifa husika ambapo
mmoja wa wazazi wake anapaswa kuwa rai wa taifa hilo.
Kifungu
hicho pia kinasema kuwa mchezaji anaweza kuwa halali endapo kati ya babu au
bibi alizaliwa katika taifa husika .
Mataifa ya Burkina
Faso , Gabon na Sudan tayari yamekutana na matatizo ya aina hiyo katika michezo
yao ya kuwania kufuzu kombe la dunia 2014.
Equatorial
Guinea kwasasa iko katika nafasi ya tatu katika kundi B wakiwa na alama tano
huku kundi hilo likiongozwa na Tunisia ambao wameshinda michezo yote mitatu ya
kundi hilo na wakiwa na alama 9.
RAFA BERNITEZ: GARY CAHILL AFANYIWA UPASUAJI
MenejaChelsea
Rafa Benitez amethibtisha kuwa mchezaji wake Gary Cahill amefanyiwa upasuaji wa
mguu.
Cahil ambaye
ana umri wa miaka 27 alienguliwa kutoka katika kikosi cha timu ya taifa ya
England maarufu kama Simba watatu kilichokuwa katika kampeni ya kufuzu kombe la
dunia dhidi ya San Marino na Montenegro, lakini pia alikuwa nje katika wa
mchezo wa ligi baina ya Chelsea dhidi ya West Ham March 17.
Cahill pia
hakusafiri kuelekea nchini Russia kwenye mchezo wa pili wa michuano ya Europa
League hatua ya robo dhidi ya Rubin Kazan ambapo pia anatarajiwa kutokuwepo uwanjani katika kipindi
kisichopungua wiki mbili.
Amekaririwa Benitez akisema
"Tulifanya hilo kwa haraka siku ya Jumamosi wakati wa mchezo dhidi ya Southampton
Machi 30"
Mlinzi huyo
wa kati wa Aston Villa na Bolton ameitumikia klabu yake jumla ya michezo 24 ya Premier
League msimu huu ambapo Benitez anadhani atafanikiwa kuponya tatizo lake kwa
haraka ambapo wakati huu atakuwa akimtegemea mlinzi mwingine Ryan Bertrand .
No comments:
Post a Comment