Na 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Mtihani
 wa uwakala wa wachezaji (players agent) na uwakala wa mechi (match 
agent) wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika 
Alhamisi ya Septemba 26 mwaka huu saa 4 kamili asubuhi kwenye ofisi za 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Kutakuwa
 na jumla ya maswali 20 kwenye mtihani huo, 15 yanatoka FIFA kuhusiana 
na kanuni za kimataifa za mpira wa miguu na matano yatatoka TFF 
kuhusiana na kanuni mbalimbali zinazotawala mchezo huo nchini.
Kwa
 ambao wangependa kufanya mtihani huo utakaokuwa katika lugha ya 
Kiingereza ambayo ni moja kati ya lugha nne rasmi za FIFA wanatakiwa 
kujisajili TFF kwa ada ya dola 50 za Marekani ambapo watapewa utaratibu 
na maeneo ambapo mtihani huo unalenga. 
Mtihani huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi, na muda wa kufanya mtihani hautazidi dakika 90.
Mpaka
 sasa Tanzania ina mawakala watano wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA. 
Mawakala hao ni John Ndumbaro, Mehdi Remtulla, Ally Saleh, Yusuf 
Bakhresa na Said Tully.
WAAMUZI VPL KUFANYA MTIHANI WA UTIMAMU WA MWILI
Waamuzi
 wote wa daraja la kwanza (Class I) wanaotaka kuchezesha Ligi Kuu ya 
Vodacom (VPL) msimu wa 2013/2014 wanatakiwa kuhudhuria mtihani wa 
utimamu wa mwili (physical fitness test) utakaofanyika katika vituo 
viwili.
Mtihani
 huo utafanyika Agosti 12,13 na14 mwaka huu katika vituo vya Dar es 
Salaam na Morogoro. Kituo cha Mwanza kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya
 Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Shinyanga, 
Simiyu, Singida na Tabora.
Kituo
 cha Dar es Salaam kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya Arusha, Dar es 
Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, 
Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.
Washiriki
 wote wanakumbushwa kuwa ni lazima wafuate utaratibu huo wa vituo, na si
 vinginevyo. Pia waamuzi waliofungiwa (sio maisha) wanatakiwa kushiriki 
katika mtihani huo.
RATIBA LIGI DARAJA LA KWANZA AGOSTI 14
Ratiba
 ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2013/2014 inayoshirikisha timu 
24 zilizo katika makundi matatu zikicheza kwa mikondo miwili (nyumbani 
na ugenini) inatarajiwa kutolewa Agosti 14 mwaka huu.
Kundi
 A linaundwa na timu za Burkina Moro ya Morogoro, JKT Mlale (Ruvuma), 
Kimondo SC (Mbeya), Kurugenzi Mufindi (Iringa), Majimaji (Ruvuma), 
Mkamba Rangers (Morogoro), Polisi (Iringa) na Polisi (Morogoro).
African
 Lyon (Dar es Salaam), Friends Rangers (Dar es Salaam), Green Warriors 
(Dar es Salaam), Ndanda (Mtwara), Polisi (Dar es Salaam), Tessema (Dar 
es Salaam), Transit Camp (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam) 
zinaunda kundi B.
Timu
 za kundi C ni JKT Kanembwa (Kigoma), Mwadui (Shinyanga), Pamba 
(Mwanza), Polisi (Dodoma), Polisi (Mara), Polisi (Tabora), Stand United 
(Shinyanga) na Toto Africans (Mwanza).
Tunapenda
 kukumbusha kuwa dirisha la usajili kwa madaraja yote ni moja ambapo 
usajili wa hatua ya kwanza ni kuanzia Juni 15 hadi Agosti 3 mwaka huu 
wakati hatua ya pili ni Agosti 14 hadi 29 mwaka huu. Dirisha dogo 
litafunguliwa Novemba 15 hadi Desemba 15 mwaka huu.
 

No comments:
Post a Comment