KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, September 26, 2013

Marco van Ginkel wa Chelsea kuwa nje ya uwanja kwa miezi sita.

Kiungo wa Chelsea Marco van Ginkel atakuwa nje ya uwanja kwa miezi sita baada ya kufanyiwa upasuaji wa mguu.
Van Ginkel, aliyehamia klabu hiyo kwa ada ya pauni milioni 8.4 akitokea katika klabu ya Vitesse Arnhem alikuwa dimbani kwa dakika 10 katika mchezo wake wa kwanza baada ya kugongwa katika mfupa wa goti na kuathirika kwa ndani.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Uholanzi alipatwa na maumivu hayo baada ya kukumbana na mchezaji wa klabu ya Swindon Alex Pritchard mapema katika mchezo wa mzunguko wa tatu wa michuano ya League One.
Chelsea imesema kuwa upasuaji wake umefanyika leo kwa ufanisiMichael Essien Chelsea
Mchezaji mwenzake Michael Essien kupitia ukurasa wake wa Twitter ameposti maneno ya 
"Stay strong Marco...you will be back stronger."

No comments:

Post a Comment