KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, November 4, 2013

Spurs wasisitiza Lloris anaweza cheza

Tottenham Hotspur wanasisitiza kuwa golikipa wao anaweza cheza licha ya kugongwa kichwa ugenini Everton kufuatia shutuma kali kwa kukosa kumwondoa uwanjani kwenye sare yao tasa Jumapili.
Spurs walikashifiwa na mkuu wa matibabu katika shirikisho la kandanda duniani, Fifa na wakereketo wa ustawi wa wachezaji kwa kukubali Lloris kubakia mchezoni licha ya mtikiso kichwani baada ya kugongana na mshambuliaji wa Everton, Romelu Lukaku.
Lakini Spurs katika taarifa walioitoa Jumatatu walisema, “Klabu kinadhibitisha kwamba Lloris alipigwa picha ya kichwa (CT Scan) na akapewa idhibati na alisafiri kurudi London (Jumapili) usiku.
“Golikipa huyo wa Ufaransa alijeruhiwa kichwani baada ya kugongana na akapewa idhini ya kuendelea na mchezo baada ya kuchunguzwa na watabibu wa klabu.”
Mkuu wa matibabu Tottenham, Wayne Diesel, aliongeza, “Baada ya uchunguzi unaofaa kutekelezwa, tuliridhika kuwa alistahili kuendelea kucheza.”
Mapema Profesa, Jiri Dvorak, ambaye ni mkuu wa matibabu Fifa, aliambia chombo cha habaro, Press Association, kuwa, “Mchezaji huyo alifaa kupumzishwa. Ikiwa mchezaji mwingine mhusika (Lukaku) alhitaji barafu kwa goti lake, inamaanisha kwamba pigo hilo lilikuwa kubwa.”
“Ni dhahiri asilimia 99 kwamba kupoteza fahamu katika tukio kama hilo kunasababisha mtikiso.”

No comments:

Post a Comment