Steven Gerrard anasema Luis Suarez huenda akaondoka Liverpool majira ya kiangazi endapo Liverpool itashindwa kufuzu kucheza Ligi ya mabingwa Ulaya.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay ambaye amefunga jumla ya mabao ndani ya ligi kuu baada ya kushuka dimbani katika michezo mitano anaonekana kuwa mwenye mashaka makubwa ya kuondoka Anfield mwishoni mwa msimu.
Itakumbukwa Suarez alishawishiwa kusalia ndani ya klabu hiyo na bosi wa Liverpool Brendan Rodgers baada ya mpango wa pauni £40 kushindwa kufikiwa na vilabu mojawapo ikiwa ni Arsenal, ambapo sasa amerejea katika kiwango chake ndani ya msimu huu.
Pia Gerrard amekaririwa akisema
'Luis yuko katika kiwango kizuri. Timu inacheza vizuri, haitakuwa tatizo mwezi Januari.
'Kiangazi ijayo, nadhani itategemea na Liverpool itafanya nini na nini kinaendelea katika mawazo ya Luis.
'Magoli yake na kiwango chake itakuwa ndio ufunguo wa kama tutamaliza katika moja ya nafasi za juu nne.'
Wakati hayo yakiwa hivyo,
Suarez anatarajiwa kuwepo katika mchezo wa Liverpool dhidi ya Fulham Jumamosi baada ya kufikia muafaka na chama cha soka cha Uruguay (UFA).
No comments:
Post a Comment