Watanzania
watatu wameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) na Chama cha
Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) ili wacheze mpira wa miguu nchini humo.
Wachezaji
hao ni Charles Mishetto na David Sondo wanaombewa hati hiyo ili waweze
kujiunga na timu ya SpVgg 1914 Selbitz, wakati Eric Magesa ameombewa
kibali hicho ili achezee timu ya klabu ya SC Morslingen.
Hata
hivyo, katika maombi hayo DFB haikuleza hapa nchini walikuwa wakicheza
katika klabu zipi. Wachezaji wote wameombewa hati hiyo kama wachezaji wa
ridhaa.
No comments:
Post a Comment