Meneja wa Uwanja wa Amani Zanzibar Khamis Ali Mzee, akimueleza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad juu ya maendeleo ya ulazaji wa nyasi bandia katika uwanja huo. |
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akitembelea uwanja wa Amani kukagua maendeleo ya kazi ya ulazaji wa nyasi bandia. (picha na Salmin Said, OMKR) |
Na Hassan Hamad OMKR
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad,
ametembelea uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar kukagua maendeleo ya zoezi la
uwekaji wa nyasi bandia katika uwanja huo.
Meneja
wa uwanja huo Khamis Ali Mzee, amesema zoezi hilo linaendelea vizuri,
huku wakiendelea kukusanya vifaa zaidi kwa ajili ya kukamilisha zoezi
hilo kwa wakati muafaka.
Amesema
vifaa vinavyoendelea kukusanywa kwa sasa ni pamoja na mchanga maalum
ambao unakwenda sambamba na uwekaji wa nyasi hizo ili kuweka umadhubuti
zaidi wa uwanja huo.
Kwa
upande wake mkandarasi wa uwekaji wa nyasi hizo bw. Ben Mushi kutoka
kampuni ya EKIKA ya Dar es Salaam, amesema mvua zinazoendelea kunyesha zinazorotesha zoezi hilo.
Hata
hivyo amesema watafanya kila juhudi kuona kuwa zoezi hilo linakamilika
kwa wakati, ili uwanja huo uweze kutumika kwa sherehe za miaka 50 ya
Mapinduzi, zinazotarajiwa kufika kilele chake tarehe 12 Januari, 2014.
No comments:
Post a Comment