KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, December 21, 2013

Luis Suarez mwiba dhidi ya Cardiff afikisha magoli 19 na kuiweka Liverpool kileleni mwa msimamo


Mshambuliaji Luis Suarez leo ameendelea kuonyesha kiwango chake katika msimu huu na kuweka Liverpool kileleni mwa ligi kuu ya England na kukifanya kibarua cha meneja wa Cardiff Malky Mackay kuwa katika wakati mgumu.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay ambaye aliwashangaza watu hapo jana kwa kusaini mkataba wa muda mrefu na klabu yake amefikisha jumla ya mabao 19 msimu akichagiza ushindi wa timu wa mabao 3-1 dhidi ya Cardiff.
Raheem Sterling pia ameiingia katika orodha ya wafungaji akifunga bao la pili licha ya kwamba Jordon alifunga bao la kufuatia machozi la Cardiff kunako dakika ya 58.
Two good: Liverpool's Luis Suarez celebrates after scoring a double against Cardiff at Anfield
Mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez akishangilia bao katika mchezo dhidi ya Cardiff uliopigwa

Matokeo hayo ya mchezo yanamuweka Mackay katika hali tete zaidi kwani tayari alikwisha kuwekwa katika tahadhari na  Vincent Tan. Mmiliki huyo wa klabu hiyo alikuwepo hii leo Anfield kushuhudia mpaka mapumziko mambo kuwa magumu kwani tayari Liverpool walikuwa wamesha kamilisha karamu yao ya magoli.
Ni mpaka lini Mackay atasalia ndani ya klabu hiyo hilo ni swali linalosubiri majibu masaa machache yajayo.
Wakitiwa mafuta na magoli ya Suarez sasa Liverpool imewapiku walikokuwa vinara kwa muda mrefu Arsenal, ambao wanatarajiwakukutana dhidi ya Chelsea Jumatatu wakati msimu ukiwa unakaribia kufikia katikati na Liverpool wakionekana kama wapinzani wakubwa wa taji msimu huu wakikimbizana vilivyo na Gunners, Manchester City na Chelsea.

Suarez sasa amefikisha jumla ya magoli 19 katika jumla ya michezo 12 aliyocheza akifunga magoli 10 katika michezo minne ya mwisho.
Unstoppable: Suarez scores Liverpool's opener with a stunning volley in the 25th minute
Make that a double: Suarez scores his second and Liverpool's third goal just before the break
Hugs: Suarez is congratulated by his team-mates after taking his goal tally for this season to 19

No comments:

Post a Comment