Moses Katabaro na Seif Ahmed wakimpokea Okwi |
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi
amewasili leo mchana majira ya saa 9:45 katika uwanja wa ndege wa
Mwalimu JK Nyererer akitokea nchini Uganda kwa shirika la ndege la
Rwanda Air.
Okwi amekuja kujiunga na timu yake mpya Yanga SC
ambayo ataanza kuitumikia katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom
na mashindano ya Kimataifa.
Mara baada ya
kuwasili JK Nyerere Okwi alipokelewa na vipngozi wa kamati ya mashindano
sambamba na washabiki, wapenzi na wadau wa soka kwa ujumla.
Okwi
akiongea na waandishi wa habari uwanja wa ndege amesema anashukuru kwa
kufika salama jijini Dar es Salaam na hasa katika timu yake mpya ya
Yanga.
Kikubwa ameahidi kucheza kwa uwezo wake wote kuhakikisha anaisaidia timu yake mpya kufanya vizuri katika mashindano yote.
Okwi
mara baada ya kuwasalimia washabiki na wanachama wa Yanga uwanja wa
Kaunda moja kwa moja ameungana na wachezaji wenzake katika kambi iliyopo
Protea kujiandaa na mchezo wa jumapili.
No comments:
Post a Comment