KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, December 20, 2013

Pep Guardiola ndiye meneja mwenye mkwanja mrefu duniani kwa mwaka. Soma orodha na malipo yao....

Meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola ndiye kocha mwenye malipo ya juu duniani.

Meneja Pep Guardiola mwenye rekodi nzuri ya kushinda mataji mawili ya klabu bingwa Ulaya (Champions Leagues) mataji matatu ya ligi kuu ya nchini Hispania (La Liga), mataji mawili ya Copa del Rey na sasa anakiongoza kikosi chenye matokeo ya ushindi mfululizo bila kupoteza katika katika kilkosi cha mabingwa wa Vilabu Ulaya Bayern Munich ndiye kocha mwenye malipo ya juu duniani.

 Pep Guardiola ndio 'best-paid football manager' duniani, akipokea pauni milioni £14.8 kwa mwaka.

Pamoja na kuwa katika hali ya kutokueleweka lakini ukweli ni kuwa kocha aliye katika wakati mgumu wa washika nyundo West Ham Sam Allardyce yeye amekamata nafasi ya 13 ya makocha wote duniani wanaolipwa vizuri kiasi cha pauni milioni £2.95 ambazo zinamuweka juu ya meneja Roberto Mancini wa Galatasaray ambaye analipwa pauni milioni £2.92, Rafa Benitez wa Napoli analipwa pauni milioni £2.92 akiwa sawa na meneja wa timu ya taifa ya England Roy Hodgson.

Kwa mujibu wa viwango vya malipo ya mishahara vilivyotolewa na jarida la 'Sporting Intelligence' limeorodhesha makocha 30 wenye malipo ya juu katika kazi za ukocha ambapo makocha nane wanatumikia vilabu vya England, watano vilabu vya Italia, wanne vilabu vya Hispania, watatu vilabu vya Ujerumani na wawili vilabu vya Urusi.

BEST-PAID FOOTBALL MANAGERS

1 Pep Guardiola, Bayern Munich, £14.8m
2 Jose Mourinho, Chelsea, £8.37m
3 Marcelo Lippi, Guangzhou, £8.34m
4 Arsene Wenger, Arsenal, £6.89m
5 Fabio Capello, Russia, £6.51m
6 Carlo Ancelotti, Real Madrid, £6.26m
7 David Moyes, Man United, £4.92m
8 Tata Martino, Barcelona, £4.5m
9 Jurgen Klopp, Borussia Dortmund, £3.59m
10 Manuel Pellegrini, Man City, £3.47m
11 Jorge Jesus, Benfica, £3.34m
12 Brendan Rodgers, Liverpool, £3.25m
13 Sam Allardyce, West Ham, £2.95m
13 Roy Hodgson, England, £2.95m
15 Roberto Mancini, Galatasaray, £2.92m
15 Rafa Benitez, Napoli, £2.92m
17 Luciano Spaletti, Zenit, £2.75m
18 Claudio Ranieri, Monaco, £2.5m
18 Laurent Blanc, PSG, £2.5m
18 Antonio Conte, Juventus, £2.5m
18 Cesare Prandelli, Italy, £2.5m
22 Massimiliano Allegri, Milan, £2.34m
23 Felipe Scolari, Brazil, £2.3m
24 Ottmar Hitzfeld, Switzerland, £2.17m
25 Mircea Lucescu, Shakhtar, £2.14m
26 Diego Simeone, Atletico Madrid, £2.09m
26 Harry Redknapp, QPR, £2.09m
26 Joachim Low, Germany, £2.09m
29 Walter Mazzarri, Inter Milan, £2m
30 Vecente del Bosque, Spain, £1.96m

Kwa wale ambao wanafundisha England huwenda isishangaze sana ambapo Jose Mourinho wa Chelsea ambaye yuko katika nafasi ya pili katika orodha nzima yeye anapokea kiasi cha pauni milioni £8.34 kwa mwaka ndani ya viunga vya vya Stamford Bridge.

Arsene Wenger wa Arsenal anapokea kiasi cha pauni milioni £6.89  yuko umbali mfupi nyuma ya Mourinho akiwa katika nafasi ya nne katika orodha ya jumla, akipitwa na kocha wa mtaliano Marcelo Lippi ambaye anakusanya pauni £8.34 akiwa na klabu ya Guangzhou. 

Meneja wa zamani wa England Fabio Capello raia wa Urusi pia ni miongoni kwa makocha wenye malipo mazuri ya mwaka akishika nafasi ya tano ambapo kwa mwaka anakusanya pauni milioni £6.51.

Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini yuko ndani ya kumi bora akikusanya kwa mwaka pauni milioni £3.47, akiwa nyuma ya Carlo Ancelotti wa Real Madrid mwenye makusanyo ya pauni milioni £6.26, David Moyes wa Manchester United ana malipo ya mwaka ya pauni milioni £4.92, huku Tata Martino wa Barcelona akikunja pauni milioni £4.5 wakati ambapo Jurgen Klopp wa Borussia Dortmund yeye akikusanya kiasi cha pauni milioni £4.3.

Not bad: David Moyes has seen a hefty wage increase since swapping Everton for Manchester United
 David Moyes
Nice work: Fabio Capello earns a large wage packet from Russia for his role as national team coach
 Fabio Capello
In the money: Sam Allardyce is 13th in Sporting Intelligence's list of best-paid bosses
Sam Allardyce nafasi ya 13
Mega-rich: Manchester City manager Manuel Pellegrini is also paid hansomely at the Etihad club
Mega-rich: meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini

No comments:

Post a Comment