Nyota wa Manchester City Yaya Toure na Sergio Aguero wamemtaka Lionel Messi kujiunga nao Etihad Stadium.
Tetesi zimeenea kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Argentine hajatulia ndani ya klabu yake ya Barcelona kufuatia Messi wiki iliyopita kumchana hadharani mkurugenzi wa klabu hiyo mbele ya makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Javier
Faus akisema mkurugenzi hajui lolote kuhusu soka.
Tatizo limeendelea kufuatia jeraha la Messi la hivi karibuni ambapo nyota huyo anayeshikilia tunzo ya Ballon D'Or kutokucheza soka tangu mapema mwezi Novemba baada ya kupata matatizo ya msuli wa paja aliyoyapata wakati wa mchezo dhidi ya Real Betis.
Akiongea na beIN
Sport, Yaya Toure amesema
'Endapo Messi ataondoka Barca? nakuja kwetu , ndio! Ningependa kusema ndio! Ndani ya Barcelona, kwa kawaida huwa kunakuwa na nyota mmoja. One. Two is not
possible.
'Majeruhi ya hivi karibuni kwa Messi na kutokuwepo uwanjani kwake kwasasa na tayari Neymar taratibu ameenza kupewa promotion, huo ni utata kwa Messi kwa kweli.'
Kwa upande mwingine mshambuliaji mwingine wa kimataifa wa Argentina Aguero ameliambia gazeto la jioni la Manchester kuwa
'Ndio, anapaswa kuja City. halafu hapo ndipo tutakapo kuwa pamoja!
City inapaswa kumnunua'
Nyota mwenza na Messi wakati huo wakiwa pamoja Barcelona Yaya Toure anataka Muajentina huyo kujiunga na Man City
Nyota mwenzie pacha Sergio Aguero ndani ya kikosi cha Argentina anamtaka Messi kuelekea Etihad.
Katika hatua nyingine baba yake na Messi, Jorge Messi mapema mwishoni mwa wiki alizima uvumi juu ya wasiwasi kuwa mtoto wake hana mapenzi na Barca kwa kusema kuwa Messi anaipenda klabu yake ya Catalan.
'Leo
amekulia Barca na anaipenda klabu yake, hakuna tatizo baina ya Leo na uongozi kwa klabu hiyo.
Kwa miezi kadhaa iliyopita Rais wa Barca Sandro Rosell amekuwa akimpa sapoti kijana huyo nyota na wanaikubali sana klabu hiyo ya Barcelona kwa namna wanavyo msapoti.
'katika kipindi kama hiki cha majeruhi tunawahitaji sana wao kuliko kipindi kingine.
Sapoti ya aina hii inaonyesha heshima wanayo mpatia Lionel.
Their aims are the same as
ours: to win as many titles as possible for the institution that we
represent.'
Nyota mwingine muajentina Argentina (pichani juu) Pablo Zabaleta, amedai kuwa Messi mara kadhaa amekuwa akimuuliza juu ya maisha ndani ya City
Messi amekuwa akifanya mazoezi huko Ezeiza ambako mara kadhaa hutumiwa na timu ya taifa ya Argentina na taarifa za kitabibu zinaeleza kuwa Messi anakaribia kuponya majeraha yake na sasa yuko katika hatua nyingine kuanza kujichanganya katika mji wa nyumbani wa Rosario.
Messi anatarajiwa kujiunga tena na kikosi cha Barcelona Januari 2 kabla ya kurejea katika kikosi cha kwanza mapema 2014.
Maoni ya Toure na Aguero yamekuwa ni kama nyongeza ya kukazia uwezekano mkubwa uhamisha ukafanyika hususani baada ya mlinzi wa wa 'Blues' Pablo Zabaleta kuweka wazi kuwa Messi amekuwaakirudia kumuuliza juu ya maisha ndani ya City.
'He asked me a lot about City, It's something we often talk about'.
No comments:
Post a Comment