KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, January 14, 2014

Coastal Union yaifunga Oman Club ya Oman bao 2-0. Fuatilia picha na stori










Mchezo ulianza saa kumi na moja alasiri kwa Wagosi kusuasua wakionekana hawajiamini, baadae walipozoeana wakaanza kupiga pasi ndefu za kutafuta bao mpaka kufika dakika ya 20 bado matokeo yalikuwa 0-0.
Ilipofika dakika ya 25, mambo yalibadilika Coastal Union walianza kupata kona na mipira ya adhabu ndogo mfululizo mpaka ilipofika dakika ya 35, Mohammed Miraji ‘Muddy Magoli’, alipofunga bao kwa njia ya kichwa baada ya kuunganisha mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Ally Nassor ‘Ufudu’, na kuwainua viongozi wa Coastal Union na maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini hapa waliokuja kushuhudia mtanange huo katika uwanja wa Nadi Oman, katikati ya jiji la Muscat.
Mpaka timu zinakwenda mapumziko matokeo yaliendelea kusomeka 1-0, ambapo mwalimu Yusuf Chipo alitumia mwanya huo kuwaeleza kuwa wapenzi wa Coastal Union wanahitaji ushindi.
Kwa upande wa kocha wa Oman Club, alitumia nafasi hiyo kubadilisha wachezaji saba na kuingiza wengine kuongeza nguvu. Hata hivyo hali ilizidi kuwa mbaya kwa upande wao ambapo mbali ya kushambulia kwa nguvu walijisahau sehemu ya katikati viungo wa Wagosi wa Kaya wakautumia mwanya huo kupiga mipira mirefu kwa washambuliaji wao.
Ilipofika dakika ya 75, kulitokea piga nikupige baada ya kona iliyochongwa na Othman Tamim, kuunganishwa na Yusuf Chuma na kuandika bao la pili huku likiwaacha midomo wazi wachezaji na viongozi wa Oman Club.
Hata hivyo ilipofika dakika ya 80 kipindi cha pili mlinzi wa Coastal Union, Marcus Ndeheli alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kupewa kadi mbili za njano, lakini kocha wa Oman Club akamuomba mwamuzi Wagosi waongeze mchezaji mwingine kwani hiyo ni mechi ya kirafiki haina haja kucheza pungufu, ndipo Kocha Yusuf Chipo akamwingiza Juma Nyoso kuchukua nafasi ya Marcus.
Mpaka mwamuzi wa leo Abdullah Al Fagry, anamaliza mechi ya leo Coastal Union, walitoka kifua mbele kwa mabao 2-0. Ambapo imeandika ushindi wa pili mfululizo baada ya awali kuwachapa Al Musannah Club mabao 2-0 yaliyofungwa na Yayo Kato na Kenneth Masumbuko.
 Baada ya mechi ya leo kocha wa Oman Club Mircea Oaida raia wa Romania, amesema ameshangazwa na uwezo ulioonyeshwa na vijana wa Coastal Union.
 “Nimeshangazwa na nidhamu ya hali ya juu iliyoonyeshwa humu ndani, ni timu nzuri ambayo inaonekana imefunzwa ikaelewa,” alisema na kuongeza.
“Nimempenda sana yule kijana mfupi namba mbili (Ayoub Masoud), anacheza kwa kujituma na ana mbio. Nimeshangazwa namna alivyo na umbo dogo lakini ameweza kuwazuia washambuliaji wangu wa pembeni mpaka wakaonekana hawachezi.”
Kikosi cha leo kilikuwa: Said Lubawa, Ayoub Masoud, Othman Tamim, Marcus Ndeheli, Yusuf Chuma, Razak Khalfan, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Ally Nassor ‘Ufudu’, Behewa Sembwana, Mohammed Miraji na Abdullah Othman ‘Ustadh’.
Baadae katika kipindi cha pili alitoka Selembe, Behewa, Ustadh, Ufudu na Mohammed Miraji. Akaingia Ayoub Semtawa, Kenneth Masumbuko, Danny Lyanga, Atupele Green na Jerry Santo.
COASTAL UNION
14 JANUARI, 2014
MUSCAT, OMAN

No comments:

Post a Comment