KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, February 19, 2014

Baba na mwana waungana kuchezea timu moja huyu ni Rivaldo na Rivaldinho dhidhi ya timu ya daraja la tatu

Rivaldo kushoto na Rivaldinho wakiichezea timu moja ya Mogi Mirim
Rivaldo ameweka historia ya aina yake kwa kucheza kiwanja kimoja na mwanae wa kiume Rivaldinho.

Mwasisi huyo wa soka wa Brazil Rivaldo ambaye kwasasa ana umri wa miaka 41, aliingia akitokea benchi akichukua nafasi katika timu yake ya Mogi Mirim katika mchezo wa ligi daraja la tatu mjini Sao Paulo (Sao Paulo State league) ikiwa ni kwa mara ya kwanza anaungana na mwanae uwanjani mwenye umri wa miaka 18.

Huo ulikuwa ni mchezo dhidi ya XV de Piracicaba uliopigwa Estadio Romildo Ferreira.
Rivaldo alishinda taji la kombe la dunia mwaka 2002 kikosi kikiwa chini ya Luiz Felipe Scolari na akiitumikia Brazil kwa michezo 74 akifunga mabao 34 kwa timu ya taifa.
Amewahi kuvichezea vilabu vya Barcelona, AC Milan, Deportivo La Coruna na Olympiakos.
Nchini Brazil amewahi kuvichezea vilabu kama Corinthians na Palmeiras kabla ya kujiunga na Mogi Mirim mwezi Disemba ambako sasa ameungana na mwanae Rivaldinho katika ligi ya daraja la tatu.
YOKOHAMA, JAPAN:  Brazil's midfielder Rivaldo hoists the World Cup trophy as the whole Brazilian team cheers after winning 2-0 against Germany in match 64 of the 2002 FIFA World Cup Korea Japan final 30 June, 2002 at the International Stadium Yokohama, Japan. Brazil has now won a record five World Cup titles.Brazil previously was a FIFA World Cup winner in 1958, 1962, 1970 and 1994. AFP PHOTO ANTONIO SCORZA (Photo credit should read ANTONIO SCORZA/AFP/Getty Images)
Rivaldo mwaka 2002

No comments:

Post a Comment