KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, March 15, 2014

Wayne Rooney: Wakumkaba mwanzo mwisho Jumapili ni Suarez kwani ni bora kama walivyo Messi na Ronaldo

Wayne Rooney anadai kuwa mchezaji ambaye amepewa kipau mbele kuzuiwa kuelekea kwenye mchezo wa kesho baina ya Manchester United dhidi ya Liverpool si mwingine bali ni Luis Suarez mchezaji ambaye anatazamwa kuwa ni miongoni mwa wachezaji bora duniani kwasasa.

United imekuwa ikifurahia ubora dhidi ya wapinzani wao hao wa zamani, katika kipindi cha karibu miongo miwili lakini msimu huu mambo yakiwaendea kombo kwani wameachwa nyuma katika msimamo wa ligi na wapinzani wao hao kutoka pande za Merseyside kwa alama 11 na ambao kwasasa wako katika nafasi ya pili katika msimamo wa Barclays Premier League.

Ukiangalia hali ya ididi ya ufungaji inaonyesha kuwa meneja wa Liverpool Brendan Rodgers ni kwamba anaonekana kufurahia mafanikio zaidi ya mwenzake wa upande wa pili David Moyes.

Liverpool imefunga jumla ya magoli 73 msimu huu ukilinganisha na United iliyoweka wavuni jumla ya magoli 46.

Mshambuliaji wa Liverpool Suarez, ambaye ameimarisha muunganiko mzuri wa safu ya ushambuliaji akiwa na Daniel Sturridge, amefunga jumla ya mabao 24 msimu huu kiasi kupelekea Rooney kuvutiwa na kiwango cha mshambuliaji huyu raia wa Uruguay.
Anakaririwa Rooney na MUTV akisema:
'Suarez, kwangu ni kwamba yuko juu kama walivyo akina Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kama wachezaji bora duniani.

Red hot! Suarez is the Premier League's leading scorer this season with 24 goals

'Amekuwa mzuri kama wawili hao katika kiwango msimu huu. tunapaswa kufanya kila linalowezekana kumzuia Jumapili.
'Nadhani wote ni wazuri na ni wazi ni vema kumuona Sturridge akifanya vizuri kwani hakuweza kuwa na nafasi katika vilabu vyake vya huko nyuma.
'Brendan Rodgers amempa nafasi na ameipokea kwa mikono miwili. Hilo ni jambo zuri pia kwa England.'

 Manchester United na Liverpool wataanza kivumbi Jumapili kwa mechi ya wakati wa maakuli ya mchana Old Trafford United wakionyesha ishara za kuimarika baada ya msimu mbaya wa kwanza chini ya meneja David Moyes.

United, ambao hawajawahi kumaliza nje ya tatu wa kwanza kwa misimu 23, hawajakuwa miongoni mwa tano wa kwanza tangu katikati ya Novemba lakini wameenda bila kufungwa wakati wa ushindi wao wa mechi mbili na sare moja mechi tatu zao zilizopita katika ligi. 

Liverpool walilaza United 1-0 uwanjani Anfield ligini Septemba 1 lakini wakashindwa nao Old Trafford katika League Cup wiki tatu baadaye. 

Wako alama 11 mbele ya United na wamo mbioni kumaliza mbele yao kwa mara ya kwanza tangu 2002.

Idadi ya ufungaji ya wakali hao watatu mpaka sasa msimu huu

                                Goals      Apps    Assists
Luis Suarez              24            23       10
Cristiano Ronaldo    24            23         7
Lionel Messi             15            20         8

No comments:

Post a Comment