KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, June 21, 2014

Raia wa Costa Rica washerehekea ushindi

Makumi ya maelfu wa raia wa Costa Rica wamesherehekea ushindi wa timu yao ya taifa katika mechi za kombe la dunia zinazoendelea nchini Brazil baada ya kuishinda italy kwa bao moja kwa bila.

Raia hao waliokuwa wakipeperusha bendera walisherehekea ushindi huo ambao umewaweka katika nafasi nzuri ya kuingia katika awamu ya mchujo kwa mara pili

Ushindi huo pia unamaanisha kuwa Uingereza imebanduliwa nje ya mashindano hayo .

Wakati huohuo Ufaransa imepanda hadi katika nafasi ya kwanza ya kundi E baada ya kuicharaza Switzerland kwa mabao matano kwa mawili.

Katika mechi za kundi jengine Ecuador iliishinda Honduras kwa mabao mawili kwa moja katika mechi iliojaa msisimuko mkubwa.

No comments:

Post a Comment