KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, June 20, 2014

Onyo kwa wakenya kuhusu kombe la dunia

Shambulizi la hivi karibuni kukumba Kenya ni la Mpeketoni ambapo watu zaidi ya sitini waliuawa
Serikali ya Kenya imewataka raiya kuwa waangalifu na kuwatahadharisha wakati huu wanapotazama michuano ya kombe la dunia.
Waziri wa usalama Joseph Ole Lenku amewataka wananchi kutazama mechi hiyo nyumbani kwao badala ya mikahawani ili kuzuia uwezekano wa kushambuliwa na wahalifu.
Hii ni baada ya kutokea mashambulizi kadhaa nchini humo na kuzorotesha hali ya usalama.
Jumapili usiku watu wasiojulikana na ambao walikuwa wamejihami walishambulia wakazi wa mji wa Mpeketoni eleo la Lamu Pwani ya Kenya na kusababisha vifo vya watu 60.
Wakazi hao walishambuliwa wakiwa wanatazama michuano ya kombe la dunia mikahwani na watu waliokuwa wamejihami kwa silaha nzito.
Malumbano yalizuka miongoni mwa wanasiasa punde baada ya mashambulizi hayo kuhusu nani aliyeyatekeleza hata baada ya Al Shabaab kukiri kuyafanya.
Shambulizi la kwanza lilitokea karibu na Lamu lilifanyika Mpeketoni wakati baadhi ya mashabiki wa soka walikuwa wakitazama mechi ya kombe la dunia.
'Tahadhari ya kwanza ''
Tangu wakati huo idara ya ulinzi ya Marekani imesisitiza kuhusu tahadhari kwa raia wake kusafiri katika eneo la pwani kwa kuhofia matukio sawa na hayo.
Ni mara ya kwanza kwa serikali ya Kenya kuwashauri raiya wake kutoenda katika maeneo ya umma ya kutazamia kombe la dunia na kuwataka wafanye hivyo nyumbani kwao.
Wakenya wengi huenda katika mikahawa kutazama mechi na ushauri huu huenda ukawakera wengi.
Taarifa hiyo inadai kuwa serikali imeimarisha usalama katika sehemu nyingi nchini mbali na kuwaagiza wamiliki wa mabaa na mikahawa kuchukua tahadhari za kiusalama ili kujiepusha na balaa.
Ushauri huo unatolewa wakati serikali nyingi zikijumuisha Marekani na Uingereza zimewatahadharisha raiya wake kusafiri katika maeneo yanayopakana nan a Somalia, Mombasa na baadhi ya sehemu za Nairobi.
Miaka minne iliyopita nchini Uganda Zaidi ya watu 70 walifariki katika shmbulizi walipokuwa wakitazama kombe la dunia na serikali ya nchi hiyo imechukua tahadari za kiusalama ili kuzuia marudio ya matukio kama hayo.

No comments:

Post a Comment