KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 11, 2014

Baada Alexis Sanchez, mzee Wenger sasa anamtaka Sami Khedira

Sami Khedira is on Arsenal's radar but the Gunners could baulk at the £20m-plus asking price
Arsenal inajaribu kufuatilia gharama nzima ya kumpata kiungo wa Real Madrid Sami Khedira.
Wakiwa tayari wameshafanikiwa kupata saini ya Alexis Sanchez, Washika mitutu sasa wammegeukia mchezaji mwingine kiungo mzuiaji  Khedira.
Khedira, ambaye amesaliwa na miezi 12 katika mkataba wake na Real, amekuwa katika kitabu cha orodha ya wachezaji wa kiungo cha mzee Arsene Wenger. 
 Klabu hiyo imekuwa ikihitaji kujua itawagharimu kiasi gani kumpata Khedira. Lakini wakati wakionekana kumkodolea macho kiungo huyo, inaonekana kuwa huenda uhamisho huo usifanyikiwe kutokana na tatizo la kifedha .
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 inaaminika kuwa huenda gharama halisi ya kunasa saini yake ikafikia pauni milioni £20 licha ya kusaliwa na miezi 12 ya mkataba ndani ya Madrid.
 Kwa kuongezea hapo Khedira mwenyewe anataka angalau kiasi cha pauni  £150,000 kwa wiki na kuwa mchezaji anayelipwa pesa nyingi Arsenal. 
Arsenal inao uwezo wa kifedha kukamilisha uhamisho huo lakini imejipanga na pauni milioni £60 kumnasa  Sanchez.
Alexis Sanchez
  Sambamba na hilo, washika mitutu pia wamekubali kulipa pauni milioni 11 kwa mlinzi wa kulia wa Newcastle Mathieu Debuchy. Na wakati Wenger akiwa katika mawindo ya mlinda mlango, mlinzi wa kati na mshambuliaji, uhamisho Khedira itakuwa ni hatua muhimu mbele.
Wenger pia anavutiwa na kiungo wa Bayer Leverkusen Lars Bender.
Mtendaji wa washika mitutu tayari amefanya mawasiliano na wakuu wa Leverkusen juu ya Bender.

No comments:

Post a Comment