KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 11, 2014

Walionunua jezi mpya ya Liverpool yenye jina na namba 7 mgongoni ya Suarez hawatarudishiwa pesa zao

Liverpool haitarudisha pesa kwa mashabiki wake ambao wamenunua jezi mpya ya klabu hiyo yenye namba na jina la Luis Suarez mgongoni baada ya mshambuliaji huyo kujiunga na Barcelona.
Suarez ameihama Liverpool na kujiunga na Barcelona kwa uhamisho wa pauni milioni 75 zikiwa ni taarifa ambazo zimethibitishwa hii leo.
Shughuli ya utengenezaji jezi ya Suarez sasa inahamia Barcelona
Kumekuwepo na fununu za karibu majuma kadhaa yaliyopita ambapo sasa hatimaye mshambuliaji huyo ametua Nou Camp.
Kumezuka malalamiko kutoka kwa mashabiki wa kweli wa klabu hiyo ambao wameanza kudai kurudishiwa fedha zao baada ya Liverpool kuwauzia jezi mpya ya Suarez mpaka mapema hii leo.
Liverpool imejibu hilo kwa kusema hakuna pesa itakayorudishwa.

No comments:

Post a Comment