KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 14, 2014

Luiz Felipe Scolari, ameacha kazi kama meneja wa Brazil

 Ripoti nchini Brazil zinasema kuwa kocha wa timu ya taifa ya Brazil,Luiz Felipe Scolari, ameacha kazi kama meneja wa timu hiyo.
Scolari alilaumiwa pakubwa sana kwa timu ya Brazil kupata kichapo kibaya ilipocheza na Ujerumani ambao wameibuka mabingwa wa kombe la dunia mwaka huu.
Kichapo hicho kilikuja wakati wa mechi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani.
Taarifa rasmi huenda ikatolewa baadaye leo na shirikisho la soka la Brazil.
Hivi karibuni Scolari alikaririwa akisema kuwa ataamua mustakabal wake baada ya kombe la dunia.
Kauli hiyo aliitoa baada ya aibu ya kutandikwa mabao 7-1 na Ujerumani katika mechi ya kwanza ya nusu fainali Jumanne iliyopita.
Vyombo vya habari vilimuandama mno kwa kichapo hicho huku mwenyewe akiahidi kutoa kauli yake baada ya mechi ya kuamua mshindi wa tatu dhidi ya Uholanzi siku ya Jumamosi ambapo waliambulia kichapo kingine cha bao 3-0.
 Kichapo cha bao 7-1 ndicho kilikuwa kibaya zaidi kuwahi kuipata Selecao tangu mwaka wa 1920 Brazil ilipolimwa 6-0 na Uruguay.
 Kocha huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 65 alikuwa ameiongoza Brazil mwaka wa 2002 lakini akondoka na kurejea mwaka wa 2012 kuiandaa timu hiyo kwa mashindano haya ya nyumbani.
Brazil walikuwa nyuma mabao 5-0 baada dakika 30 ya kipindi cha kwanza kabla ya kukamilisha mechi hiyo mabao 7-1.

No comments:

Post a Comment