KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, July 3, 2014

Mjumbe wa Fifa Houlier ataka wachezaji watatu waongezwe hatua robo fainali kombe la dunia

Mjumbe wa kamati ya Ufundi ya shirikisho la soka duniani kote FIFA Gerard Houlier anatarajiwa kuwasilisha hoja binafsi ya kutaka kanuni za mabadiliko ya wachezaji za michuano ya shirikisho hilo zibadilishwe kutokana na tathmini aliyoifanya kwenye fainali za kombe la dunia zinazoendelea nchini Brazil kwa sasa.

Houlier ambaye anakumbukwa na mashabiki wa soka duniani kote kufuati mchango wake alioutoa wakati wakiwa meneja wa klabu ya Liverpool ya nchini Uingereza, anejipanga kuwasilisha hoja hiyo kwenye kamati ya ufundi kabla ya kufikishwa kwenye mkutano mkuu ujao wa FIFA.


Babu huyo mwenye umri wa miaka 66, ameshawishika kuwasilisha hoja binafsi kwenye kamati ya ufundi ya FIFA baada ya kubaini ipo haja kwa timu zinazofika kwenye hatua ya mtoano kupewa ruhusa ya kufanya mabadiliko ya wachezaji zaidi ya watatu.

Amesema katika fainali za mwaka huu, baadhi ya timu ambazo ziliingia kwenye hatua ya mtoano zilikabiliwa na mtihani wa kucheza pungufu kwa dakika kadhaa kutokana na wachezaji kuumia, na wakati mwingine wachezaji walionekana wakiwa wamechoka, hivyo anahisi ipo haja kwa FIFA kutoa nafasi kwa makocha kufanya mabadiliko angalau kwa mchezaji mmoja.

Hata hivyo Gerard Houlier amesisitiza hoja yake itahusisha michezo ambayo itaongezewa dakika 30 endapo mshindi hatopatikana ndani ya dakika 90.

Akitolewa mfano wa mchezo wa Ubelgiji dhidi ya Marekani Houlier amesema mshindi wa mpambano huo alipatikana baada ya faida ya mchezaji wa akiba Lomelo Lukaku, aliyeingizwa katika dakika 30 za mwisho ili hali kwa upande wa Marekani kocha Jürgen Klinsmann alikuwa ameshamaliza idadi ya wachezaji wa akiba kutokana na baadhi yao kuumia kabla ya kuongezwa kwa dakika 90.

No comments:

Post a Comment